Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka kati ya Handeni na Kilindi katika eneo la Bondo?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kupata maswali mawili ya nyongeza.
La kwanza, mara baada ya mgogoro huo kutatuliwa, Shule ya Msingi Bondo iliyokuwa Handeni Mjini tumeikabidhi Kilindi, na Shule ya Msingi Parakwiyo iliyokuwa Kilindi imekabidhiwa Handeni Mjini. Swali langu ni kwamba, ni lini sasa Sereikali itaweka utaratibu wa walimu wa shule hizi mbili kuhamishiwa kwenye halmashauri husika?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuambatana na mimi mara baada ya Bunge hili kwenda Kata ya Kwamagome kwenye eneo linaloitwa Kwaubaka ambako sasa baada ya kuikabidhi Shule ya Msingi Bondo kwenda Kilindi, tumeanza jitihada za kujenga shule nyingine ili akajionee jitihada za wananchi na waone namna gani Serikali watatusaidia?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Kwagilwa, kama ifuatavyo; kwanza, niwapongeza Wananchi wa Halmashauti ya Handeni pamoja na Kilindi kwa kutatua mgogoro huu na nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kusimamia suala hilo kwa umakini mkubwa.

Mheshimiwa Spika, nimuhakikishie tu kwamba tumeshatoa maelekezo kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, kuhakikisha ifikapo tarehe 30 Desemba mwaka huu Watumishi wote wa shule ya Bondo na Parakwiyo wawe wamepewa barua zao za uhamisho kulingana na eneo ambalo wanatakiwa kuwa katika halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Spika, pili, niko tayari kuambatana na Mheshimiwa Mbunge kwenda kuona juhudi za wananchi na kuona namna gani Serikali itawaunga mkono. Ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka kati ya Handeni na Kilindi katika eneo la Bondo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Mgogoro kati ya mpaka wa Mkoa wa Singida na Mkoa wa Tabora kwenye Wilaya za Uyui na Sikonge upo tangu mwaka 2002 na mwaka 2009 wataalamu walikubaliana kuchora upya huo mpaka. Sasa je, ni lini Serikali itaweka hizo beacons kutenganisha hii mipaka ya Mkoa wa Tabora na Mkoa wa Singida ili kuondoa hiyo migogoro?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Natumia fursa hii kuwaelekeza Wakuu wa Mikoa ya Tabora na Singida kuhakikisha wanatekeleza maelekezo ya Serikali ya kutatua migogoro ya mipaka kati ya wilaya na wilaya, lakini kati ya mkoa na mkoa ili wananchi waweze kufanya kazi kwa utulivu na amani.

Mheshimiwa Spika, tutafuatilia hilo kwa Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa hii miwili, nakuhakikishia kwamba Ofisi ya Rais TAMISEMI, itahakikisha beacons hizo zinawekwa na kuhakikisha kwamba wananchi wanatambua mipaka yao na kufanya kazi zao kwa amani. Ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka kati ya Handeni na Kilindi katika eneo la Bondo?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa hii fursa. Tatizo la mpaka lipo kule kwetu kati ya Wilaya ya Arumeru Mashariki, Hai na Siha, eneo lile linasemekana ziko GN kama tatu. Je, Serikali inasemaje kuhusu mpaka halisi wa Arumeru Mashariki, Siha na Hai?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Utaratibu wa mipaka unaainishwa kwa mujibu wa GN zinazotambullika rasmi na Serikali. Kiutaratibu GN ya mwisho ndiyo GN ambayo inatambulika, GN ambayo imepitishwa kwa mara ya mwisho ndiyo GN ambayo ina-sound kwa kipindi hicho.

Mheshimiwa Spika, naomba nichukue jambo hili la Mheshimiwa Pallangyo ili tuweze kuongea na Mkuu wa Mkoa wa Arusha lakini na Kilimanjaro ili waweze kuona namna nzuri ya kwenda na wataalamu kusoma GN uwandani, kutafsiri mipaka ya Wilaya ya Hai, Siha Pamoja na Arumeru Mashariki ili wananchi watambue mipaka hiyo lakini pia waweze kufanya shughuli zao kwa amani zaidi, ahsante.