Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 126 2023-11-09

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka kati ya Handeni na Kilindi katika eneo la Bondo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer


NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilikwisha tatua mgogoro wa mpaka kati ya Halmashauri ya Mji wa Handeni na Kilindi katika eneo la Bondo kwa maelekezo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga kwenye kikao cha tarehe 25 Julai, 2023.

Mheshimiwa Spika, timu ya wataalam wa ardhi, Wajumbe wa Kamati za Ulinzi na Usalama wa Wilaya na viongozi ngazi ya Tarafa, Kata na Vijiji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi na Handeni walikutana tarehe 8 – 9 Oktoba, 2021 kwa ajili ya kupitia Tangazo la Serikali (GN), kuhakiki idadi ya watu, kuhakiki upatikanaji wa huduma za kijamii pamoja na kutoa ushauri wa kitaalam ambapo taarifa hiyo iliwasilishwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa utekelezaji.

Mheshimiwa Spika, Wakurugenzi wa halmashauri ya Kilindi na Handeni wameelekezwa kutekeleza masuala yafuatayo; kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa uhifadhi wa misitu, kuheshimu mpaka ulioainishwa kutokana na tafsiri sahihi ya matangazo ya Serikali, kurekebisha usajili wa shule za Msingi Bondo na Parakwiyo ili zisomeke ndani ya Wilaya husika, ahsante.