Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 719 2023-06-26

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, lini Serikali itapandisha hadhi barabara ya Kwinji - Kilindi Asilia hadi Kimbe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Jimbo la Kilindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kwinji - Kilindi Asilia hadi Kimbe ina urefu wa kilometa 43.7, barabara hii inaanzia Kata ya Msanja, inapita Makao Makuu ya Kata ya Kilindi Asilia na kuunganisha Kata ya Kimbe.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Barabara Namba 13 ya mwaka 2007, Kifungu cha 11 na Kanuni za Usimamizi wa Barabara ya mwaka 2009 kifungu 43(1) na (2) na kifungu 44(1), kupitia Tangazo la Serikali Na. 21 ya tarehe 23 Januari, 2009 imeainisha vigezo vya utaratibu wa kuhamisha barabara ili iwe chini ya TANROADS ambapo barabara inaweza kupandishwa au kuteremshwa kutoka daraja moja kwenda daraja jingine. Mkoa unashauriwa kuwasilisha mapendekezo ya kupandisha hadhi barabara hiyo kwenye Bodi ya Barabara ya Mkoa ili utaratibu ufuatwe.