Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 681 2023-06-21

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: -

Je, ni nyumba ngapi zinahitajika kwa Watumishi wa Umma waliopo Vijijini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEORGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shally Josepha Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimwa Mwenyekiti, ni kweli kuna uhitaji mkubwa wa nyumba za watumishi waliopo vijijini hususan watumishi wa kada ya elimu na afya. Hadi Mei, 2023, idadi ya nyumba za walimu zilizopo vijijini ni 55,097 wakati upungufu ni nyumba 255,097. Aidha, kwa upande wa watumishi wa afya, nyumba za watumishi zilizopo ni 7,818 na upungufu ni nyumba 15,272.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 kupitia Mradi wa SEQUIP, Serikali imekamilisha mchakato wa kujenga nyumba 212. Serikali itaendelea na jitihada za kukabiliana na upungufu wa nyumba za watumishi wa kada za elimu na afya hususan waliopo vijijini.