Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 559 2023-06-08

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kuchukua hatua kwa Watumishi wanaoripoti na kuondoka bila kufanya kazi Wilayani Tunduru?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ilikwishatoa waraka wa kusimamia masuala ya uhamisho wa watumishi kutoka mwajiri mmoja kwenda mwingine ikiwemo Mamlaka za Serikali za Mitaa ambapo Waraka huo pamoja na mambo mengine, unaelekeza Mtumishi wa Umma kukaa kwenye kituo chake cha kazi kwa muda usiopungua miaka mitatu kabla ya kuomba kibali cha kuhama kwenda katika kituo kingine cha kazi.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kusimamia utaratibu huu ili kuhakikisha kuwa watumishi wanaopangiwa vituo vya kazi ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru wanafanya kazi katika vituo vyao.