Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 558 2023-06-08

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kujenga nyumba za walimu Shule za Msingi katika Kata za Salale, Kiongoroni, Mbuchi na Maparoni Kibiti?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Subira Khamis Mgalu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uhitaji wa nyumba za walimu hususan katika maeneo ya visiwani na imeendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kutatua changamoto hiyo. Katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, Serikali ilitenga shilingi bilioni 55.57 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu 809 zenye uwezo wa kuchukua kaya 1,916.

Mheshimiwa Spika, kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti, Kata za Maparoni na Kiongoroni ambazo zipo visiwani, Serikali imepeleka shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba mbili za walimu (2 in 1) katika Shule za Msingi Maparoni na Jaja na taratibu za ujenzi wa nyumba hiyo zinaendelea.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu hususan katika maeneo ya pembezoni ikiwemo katika Visiwa vya Kata za Salale, Kiongoroni, Mbuchi na Maparoni Kibiti.