Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 40 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 528 2023-06-05

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa ujenzi wa vizimba vya ufugaji wa samaki katika Ziwa Duluti?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvivu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ziwa Duluti ni sehemu ya Hifadhi ya Msitu wa Asili wa Ziwa Duluti ambao unasimamiwa na Wakala ya Huduma za Misitu (TFS). Hifadhi hiyo ni kivutio cha utalii wa ikolojia, picha, kutembea msituni, kuangalia ndege na viumbe wengine, boti za kupiga kasia na uvuvi wa burudani. Kutokana na hadhi ya eneo tajwa, shughuli za kiuchumi zinadhibitiwa ili kutokuharibu ikolojia na bioanuwai iliyopo katika eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumuahidi Mheshimiwa John Danielson Pallangyo Mbunge, kuwa katika mwaka wa fedha 2023/2024 Wizara yangu itafanya utafiti kupitia Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi TAFIRI kwa kushirikiana na TFS ili kuona kama ufugaji wa Samaki wa vizimba unaweza kufanyika bila kuathiri ikolojia na bioanuai katika Ziwa Duluti.