Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 464 2023-05-29

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza:-

Je, Serikali imejipangaje kusimamia ubora wa nguo na viatu vya mtumba vinavyotoka nje ya nchi ambavyo havina ubora na bei ni kubwa?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Moshi Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Shirika la Viwango Tanzania inatekeleza majukumu ya udhibiti wa ubora na usalama wa bidhaa zinazoingia na kutoka nchini kupitia Kitengo cha Udhibiti wa Ubora wa Bidhaa zinazoingia na kutoka nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bidhaa zote zinazotoka nje ya nchi zilizoainishwa kwa vigezo mbalimbali zikiwemo nguo na viatu vya mtumba hukaguliwa chini ya mfumo wa ukaguzi wa shehena kabla ya kuingia nchini (Pre-Shipment Verification of Conformity to Standards), ukaguzi ambao unafanywa na mawakala waliopewa dhamana na shirika. Pamoja na kukagua ubora, vilevile usalama wa nguo na viatu vya mitumba hukaguliwa kwa vigezo vya kiafya na kutoa cheti cha afya (Fumigation Certificate). Endapo bidhaa hizo zitakidhi vigezo vilivyowekwa na kuhakikiwa na Maafisa Afya, pale shehena husika inapofika bandarini Dar es Salaam au katika mpaka wowote, nashukuru.