Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 132 2023-09-08

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: -

Je, lini barabara ya Ulinzi ya Hifadhi ya Mwalimu Nyerere inayojengwa toka Liwale hadi Mahenge itakamilika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamedi Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kutambua umuhimu wa barabara hii kiulinzi na kijamii na inayounganisha Mikoa ya Lindi na Morogoro, katika mwaka wa fedha 2023/2024 jumla ya shilingi milioni 143.04 zimetengwa kwa ajili ya kazi za upembuzi yakinifu wa awali. Kazi ya upembuzi yakinifu wa awali itakapokamilika katika barabara hii inayopita katika Hifadhi ya Mbuga ya Wanyama ya Selous, itaonesha iwapo mradi unakidhi vigezo vya uhifadhi mazingira ili kuwezesha kujengwa, ahsante.