Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 33 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 438 2023-05-25

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: -

Je, lini Bandari ya Karema itafunguliwa na kuanza kufanya kazi kwa kuwa ujenzi umekamilika kwa asilimia 87?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania imeshakamilisha ujenzi wa Bandari ya Karema na huduma katika bandari hiyo zimeanza kutolewa rasmi kuanzia tarehe 1 Septemba, 2022 baada ya kufanyiwa uzinduzi na Mkuu wa Wilaya ya Ziwa Tanganyika. Bandari hiyo inahudumia abiria na shehena mbalimbali za ndani ya nchi na zile zinazosafirishwa kati ya Tanzania na nchi jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.