Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 391 2023-05-22

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga campus ya Chuo Kikuu Mzumbe katika Mkoa wa Singida?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na mpango wa kupeleka huduma ya elimu ya juu katika mikoa isiyokuwa na Chuo Kikuu au Taasisi ya Elimu ya Juu ukiwemo Mkoa wa Singida. Kwa sasa Serikali kupitia Mradi wa Higher Education for Economics Transformation (HEET) imetenga jumla ya Dola za Kimarekani milioni nane kwa ajili ya upanuzi na ukarabati wa Kampasi ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) katika Mkoa wa Singida. Maandalizi ya shughuli za ujenzi yameshaanza ambapo hadidu za rejea za kumpata Mshauri Elekezi na Mkandarasi, Michoro na Mpango kabambe wa Ripoti ya Tathmini ya mazingira na Jamii (Environmental and Social Impact Assessment) vimeshaanza kuandaliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jitihada hizo za kusogeza elimu ya juu kwenda mikoa ambayo haina taasisi hizo, Chuo Kikuu cha Mzumbe pia kupitia mradi wa HEET kimepangiwa kujenga kampasi mpya katika Mkoa wa Tanga katika Wilaya ya Mkinga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.