Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 27 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 354 2023-05-17

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Matala – Mwanhuzi – Lalago kwa kiwango cha lami?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Tlemai Awack, Mbunge wa Karatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya barabara ya Matala – Mwanhuzi – Lalago yenye kilometa 148.4 ya kutoka Lalago – Mwanhuzi – Sibiti – Nyahaha imo kwenye mradi wa ujenzi wa Barabara ya Maswa – Lalago - Sibiti River – Haydom – Mbulu – Karatu yenye urefu wa kilometa 339 ambao utatekelezwa kwa utaratibu wa Engineering, Procurement and Construction plus Financing (EPC+F) ambao hadi sasa mkandarasi amepatikana na mkataba wa ujenzi utakuwa umesainiwa kabla ya mwishoni mwa mwezi Juni, 2023. Kwa sehemu ya Nyahaha kwenda Matala (kilometa 25) Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami, ahsante.