Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 23 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 300 2023-05-11

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: -

Je, ni lini ukarabati utafanywa katika njia ya umeme kutoka kituo kikubwa kuelekea Ikungi, Manyoni, Itigi, Mitundu hadi Mwamagembe?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Singida umeunganishwa na Gridi ya Taifa kutoka katika kituo cha kupoza umeme kilichopo Mkoani Dodoma kupitia njia ya kusafirisha umeme za msongo wa kilovolti 220 na 400 hadi kituo cha kupoza umeme cha Singida. Kwa kutumia msongo huo mkubwa, Serikali kulingana na upatikanaji wa fedha imepanga kujenga kituo kikubwa cha kupoza umeme Wilayani Manyoni ili kuondoa changamoto za umeme kusafiri umbali mrefu.

Mheshimiwa Spika, matengenezo ya njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 33 kutoka kituo kikubwa cha kupoza umeme cha Singida kuelekea Manyoni, Itigi, Mitundu hadi Mwamagembe tayari yanaendelea na katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetenga kiasi cha shilingi 471,000,000.00 kwa ajili ya matengenezo ya njia hiyo. Vilevile mkandarasi wa njia ya reli ya SGR atakapomaliza ujenzi eneo la Kintinku, TANESCO itaunganisha njia ya umeme kutoka Wilaya ya Bahi kwenda Manyoni, hivyo kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo hayo.