Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 23 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 295 2023-05-11

Name

Salim Alaudin Hasham

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga kwa kwango cha lami barabara ya kutoka Ifakara hadi Mahenge?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Salim Alaudin Hasham, Mbunge wa Ulanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Ifakara Kibaoni hadi Mahenge Mjini yenye urefu wa kilometa 55.4 ni sehemu ya Barabara ya Ifakara – Mahenge– Malinyi – Kilosa kwa Mpepo
– Londo hadi Lumecha yenye urefu wa kilometa 435 ambayo Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) tayari imetangaza zabuni kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa utaratibu wa EPC+F. Uchambuzi na tathmini ya zabuni za kumpata Mkandarasi na Mwekezaji atakayetekeleza mradi huu zinaendelea na zinatarajiwa kukamilika kabla ya mwisho wa Juni, 2023, ahsante. (Makofi)