Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 22 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 290 2023-05-10

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWATUMU DAU HAJI aliuliza: -

Je, lini Serikali itaongeza gari lingine la polisi wilaya ya Kusini Unguja kwani gari moja lililopo halikidhi mahitaji?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwatumu Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi wilaya ya Kusini Unguja, katika mkoa wa kusini Unguja una magari manne ambayo yote ni mazima na yanatumika kutoa huduma katika eneo hilo. Magari hayo ni PT 4807 Ashok Leyland ambalo liko kituo cha Polisi Kizimkazi, PT 4808 Ashock Leyland ambalo liko Kituo cha Polisi Paje, PT 1906 Toyota Land Cruiser ambalo lipo Kituo cha Polisi Paje, PT 3860 Toyota Hilux Double Cabin ambalo liko kituo cha Polisi cha Wilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia bajeti yake ya mwaka wa fedha 2022/2023 imetoa kiasi cha fedha shilingi billioni 15 kwa ajili ya Jeshi la Polisi ili kununulia pikipiki pamoja na magari ambayo yamepangwa kugawiwa kwenye mikoa na wilaya zote nchini.