Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 54 2023-04-12

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kupeleka watumishi na vifaa tiba katika Kituo cha Afya Majengo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Jimbo la Nanyamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua changamoto ya uhaba wa Wataalam wa afya katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini. Hata hivyo, Serikali imeendelea kutoa vibali vya kuajiri Watumishi wa Kada ya Afya katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2020/2021 na 2021/2022, Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI iliajiri Watumishi wa Kada za Afya 10,328 ambapo Halmashauri ya Mji Nanyamba ilipata watumishi 51 wa kada mbalimbali za afya. Aidha, Kituo cha Afya Majengo kilipangiwa watumishi wanne ambao ni Mteknolojia wa Maabara, Tabibu Msaidizi na Wauguzi wawili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imepeleka vifaa na vifaa tiba katika Halmashauri ya Mji Nanyamba vyenye thamani ya shilingi milioni 300 kwa ajili ya vituo vya huduma za afya, ahsante.