Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 57 2023-04-12

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Masasi – Nachingwea kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri Waziri Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cecil David Mwambe, Mbunge wa Ndanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Masasi – Nachingwea yenye urefu wa kilometa 45 ni sehemu ya barabara ya Masasi – Nachingwea – Liwale yenye urefu wa kilometa 175 ambayo ipo katika hatua ya Manunuzi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa kutumia utaratibu wa EPC+F. Uchambuzi wa zabuni upande wa technical umekamilika na sasa unafuata uchambuzi wa financial ambao utafanywa na Wizara ya Fedha na Mipango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)