Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 24 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 214 2022-05-17

Name

Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuajiri Askari wa Jeshi la Polisi katika Mkoa wa Kusini Pemba?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ramadhan Suleiman Ramadhan Mbunge wa Chakechake, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali imetoa kibali cha kuajiri askari wapya wa Jeshi la Polisi 4,103. Kwa sasa askari hao wapo kwenye mafunzo ya awali katika shule ya Polisi Moshi. Watakapomaliza mafunzo yao, watagawiwa kwenye maeneo yenye upungufu mkubwa wa askari ikiwemo mkoa wa Kusini Pemba. Nashukuru.