Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 12 2023-04-04

Name

Ameir Abdalla Ameir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR K.n.y. MHE. AMEIR ABDALLAH AMEIR aliuliza: -

Je, Balozi za Tanzania zinatumia mikakati gani kutangaza bidhaa za Tanzania Kimataifa?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ameir Abdallah Ameir, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001 inatoa msisitizo katika utekelezaji wa diplomasia ya uchumi ambayo lengo kuu ni kujenga, kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi yetu. Kwa muktadha huo, balozi zetu nje ya nchi, zimeendelea kubuni mikakati mbalimbali katika kutekeleza vyema diplomasia ya uchumi kwa kutangaza bidhaa na huduma zinazozalishwa nchini ikiwa ni pamoja na masoko ya bidhaa na huduma hizo.

Mheshimiwa Spika, mikakati hiyo ni pamoja na kuratibu na kufanikisha upatikanaji wa vibali/ithibati kwa kampuni za Tanzania kuuza bidhaa zao katika masoko ya nje; kuratibu na kushiriki katika makongamano ya biashara, maonesho na mikutano ya kimataifa ndani na nje ya nchi; kuratibu na kufanikisha ziara za wawekezaji na wafanyabiashara kutoka nje ya nchi; Kuratibu na kufanikisha ziara za kuutangaza utalii (road show), watu maarufu na mashuhuri, kampuni za kitalii na Kubidhaisha lugha ya Kiswahili na kuitangaza kimataifa, ahsante sana.