Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 65 2023-02-03

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuinua ushiriki wa Watu wenye Ulemavu katika michezo ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa wavu na pete?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Khadija Shaaban Taya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikitoa haki sawa ya ushiriki katika michezo kwa makundi yote ikiwemo watu wenye ulemavu. Moja ya mikakati ya Serikali katika kuinua ushiriki wa watu wenye ulemavu hususani kwenye mpira wa miguu, wavu na pete ni pamoja na kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa kushirikisha watu wenye ulemavu katika michezo, kusajili vyama na vilabu vya michezo kwa watu wenye ulemavu, kushirikisha michezo ya watu wenye ulemavu katika matukio yote ya michezo hususani yanayoandaliwa na Serikali, hii ni pamoja na kuziwezesha timu za Taifa za watu wenye ulemavu zinaposhiriki katika mashirikisho mbalimbali ya Kimataifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali kwa kushirikiana na wadau wa michezo imeendelea kuhamasisha ujenzi wa miundombinu ya michezo yenye mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu.