Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 9 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 137 2022-11-10

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje katika kupambana na changamoto ya upungufu wa Wataalam wa Mazoezi Tiba na huduma ya Utengamao nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alice Karungi Kaijage, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeajiri jumla ya wataalam 84 wa mazoezitiba na huduma mtengamao katika ajira za mwezi Julai, 2022. Hata hivyo, kufanya idadi ya wataalam wa mazoezitiba na huduma mtengamao kuongezeka kutoka 653 hadi 737.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa kuna jumla ya vyuo vikuu vinne ambavyo ni Muhimbili, KCMC, Bugando na Zanzibar vinavyotoa taaluma, hivyo kupunguza changamoto ya uwepo wa wataalam katika soko la ajira.