Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 39 Energy and Minerals Wizara ya Madini 328 2021-05-28

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itafikisha umeme katika vijiji 28 ambavyo bado havijapata umeme kati ya vijiji 50 vya Jimbo la Singida Mashariki?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu, Mbunge wa Singida Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kupeleka umeme vijijini na kuufikisha katika vijiji vyote vya Tanzania Bara ifikapo mwezi Desemba, 2022.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Singida Mashariki lina jumla ya vijiji 50. Vijiji 22 tayari vina umeme; vijiji 12 vinapatiwa umeme sasa kupitia Mradi wa Ujazilizi (Densification) ulioanza kutekelezwa katika Mkoa wa Singida mwezi Novemba, 2020 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2021.

Mheshimiwa Spika, vijiji 16 vilivyobakia vinaendelea kupatiwa umeme kupitia utekelezaji wa Mradi wa REA wa kusambaza umeme vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili ulioanza kutekelezwa mwezi Machi, 2021 na utakaokamilika mwezi Desemba, 2022. Gharama ya mradi ni bilioni 8.47.