Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 98 2021-02-10

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI Aliuliza:-

Je, ni lini ahadi ya Serikali ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Lushoto – Muyanta hadi Mlalo itaanza kutekelezwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Lushoto – Mlalo yenye urefu wa kilometa 41.93 ni sehemu ya Barabara ya Lushoto – Mlalo – Umba junction yenye urefu wa kilometa 66.23 ambapo kati ya hizo, kilometa tisa ni za lami na kilometa 32.93 ni za changarawe. Katika mwaka wa fedha wa 2020/ 2021 kiasi cha milioni 420 zimetengwa kutoka Bodi ya Mfuko wa Barabara kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa mita 400 za barabara hii kwa kiwango cha lami. Ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu zilizobaki utaendelea kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Barabara ya Lushoto – Mlalo – Umba Junction kiuchumi, kiulinzi na kiutalii na hivyo wakati ujenzi kwa kiwango cha lami kwa awamu ukiendelea, Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya matengenezo mbalimbali kila mwaka. Katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 jumla ya Shilingi milioni 475.5 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo ili kuhakikisha kuwa barabara hiyo inapitika majira yote ya mwaka.