Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 46 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 383 2019-06-17

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:-

Katika Jimbo la Korogwe Vijijini bado vijiji vingi havina umeme.

Je, ni lini usambazaji wa umeme kupitia REA utakamilika katika vijiji vya Jimbo la Korogwe Vijijini?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kutekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vijiji vyote nchini hadi ifikapo mwezi Juni, 2021. Katika Jimbo la Korogwe Vijijini jumla ya vijiji 71 vitaunganishiwa umeme. Aidha, vijiji 14 vya Hamashauri ya Wilaya ya Korogwe Vijijini vinatarajiwa kupatiwa umeme kupitia Mradi wa REA III mzunguko wa kwanza unaoendelea kutekelezwa. Hadi kufikia mwezi Juni, 2019 Mkandarasi Kampuni ya DERM Electrics ameshawasha umeme katika vijiji vinne vya Nkalekwa, Magila, Kwasunga na Welei pamoja na kuunganisha umeme kwa wateja wa awali zaidi ya 112.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa mkandarsi anaendelea na kazi ya kusimika nguzo, kuvuta nyaya na kufunga transifoma katika vijiji kumi vitakavyopatiwa umeme kupitia mradiwa REA lll mzunguko wa kwanza. Kazi za mradi katika Jimbo la Korogwe Vijijini zinahusisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 9.45, njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 48 na ufungaji wa transfoma 18 za kVA 50 na 100, pamoja na kuunganisha umeme kwa wateja wa awali 825 na gharama za mradi ni shilingi bilioni moja na milioni 600.

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vilivyosalia 57 vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA III mzunguko wa pili, unaotarajiwa kuanza mwezi Julai, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2021.