Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 14 Energy and Minerals Wizara ya Madini 119 2019-04-23

Name

Prosper Joseph Mbena

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:-

(a) Je, ni lini Serikali itafanya utafiti wa uhakika katika Vijiji vyote vya Jimbo la Morogoro Kusini ili kubaini madini yaliyopo?

(b) Je, Serikali itawasaidiaje Wachimbaji wadogo wa Rubi, Spinel na Dhahabu ili waweze kuzalisha zaidi na kupata masoko ya uhakika?

(c) Je, ni lini Serikali itatuma Wataalam wa kuthibitisha wingi wa madini ya Graphite na Chokaa katika maeneo ya Jimbo la Morogoro Kusini ili mipango ya kuchimba iweze kuanza?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Prosper Joseph Mbena, Mbunge wa Morogoro Kusini, lenye vipengele (a), (b) na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mwaka 2014, Serikali kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) ilifanya utafiti wa awali wa kijiolojia katika Jimbo la Morogoro Kusini na kutengeneza ramani ya kijiolojia (Quarter Degree Sheet – QDS) zipatazo tisa.

Mheshimiwa Spika, taasisi kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ikiwemo kampuni ya Beak Consultants ya Ujerumani na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kati ya mwaka 2013 na 2014 walifanya utafiti wa awali na kubainisha uwepo wa madini ya dhahabu katika Kata za Mkuyuni, Mikese, Mazimbu, Kisemu na Tununguo; vilevile madini ya chokaa katika Kata ya Mkuyuni na Kisaki; madini ya Kinywe (graphite) katika Kata za Mvuha, Mkuyuni, Kisemu na Mtombozi.

Mheshimiwa Spika, aidha, utafiti huo ulibainisha pia uwepo wa madini ya ruby katika Kata za Tawa, Mkuyuni na Mkambalani. Vilevile kuna madini ya spinel na barite katika Kata za Mkuyuni.

Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali za Madini (SMMRP) imenunua mtambo wa kuchoronga miamba mipya na kuikabidhi katika Shirika la (STAMICO) kwa lengo la kufanya utafiti katika maeneo ya wachimbaji wadogo kwa gharama nafuu.