Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prosper Joseph Mbena

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itafanya utafiti wa uhakika katika Vijiji vyote vya Jimbo la Morogoro Kusini ili kubaini madini yaliyopo? (b) Je, Serikali itawasaidiaje Wachimbaji wadogo wa Rubi, Spinel na Dhahabu ili waweze kuzalisha zaidi na kupata masoko ya uhakika? (c) Je, ni lini Serikali itatuma Wataalam wa kuthibitisha wingi wa madini ya Graphite na Chokaa katika maeneo ya Jimbo la Morogoro Kusini ili mipango ya kuchimba iweze kuanza?

Supplementary Question 1

MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri sana ya swali hili; na kwa kweli ni majibu sahihi. Napenda tu niulize maswali madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza, yapo maeneo ambayo hayakutajwa hapa ambayo ni Dutumi Bwakila Chini, wana dhahabu na ruby; Konde wana dhahabu na gemstone, hiyo spinels; pia Singisa wana ruby ya kutosha. Sasa swali langu la msingi kwa maana ya yale yaliyojibiwa yajumuishwe na maeneo haya mapya ili sasa tuweze kupata uhalisi wa sehemu ambazo madini haya yanapatikana. Hili ni ombi tu.

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Je, Serikali ina utaratibu gani kuwasaidia hawa wachimbaji wadogo kifedha pamoja na vifaa kwa ajili ya kuboresha uchimbaji wao?

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna maeneo ambayo hayajatajwa. Maeneo ambayo tumeyataja ni yale maeneo ambayo tumeona ni potential kwa uchimbaji. Vile vile nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo yote ya Morogoro tunayafahamu na tumetengeneza ile Quarter Degree Sheet ambayo inaonesha ramani zote za uwepo wa madini.

Mheshimiwa Spika, vile vile uwepo wa madini ni kitu kimoja, lakini madini yanayolipa automatically tu utaona kwamba wachimbaji wanaelekea katika maeneo yale. Ni kama vile inzi anavyofuata kidonda; wachimbaji wakishaona kuna potential maeneo ya uchimbaji, wenyewe unaona wameshasogea pale.

Mheshimiwa Spika, kwa uchambaji ule mkubwa inabidi utafiti wa kina ufanyike na pawe na ile hali ya kuonesha kwamba kuna madini ya kutosha na hata uwekezaji mkubwa unaweza ukawekezwa pale. Kwa wachimbaji wadogo wana uwezo wa kusogea na tuko tayari kuwasaidia kuendelea kuwapa taarifa za kijiolojia.

Mheshimiwa Spika, napenda tu kusema kuhusiana na kuwawezesha wachimbaji wadogo; Wizara imekuwa bado inasaidia kuwawezesha wachimbaji wadogo. Hapo nyumba tulikuwa katika huo mradi wa SMMRP, tulikuwa tunatoa ruzuku kwa wachimbaji wadogo, lakini ruzuku hiyo ilikuwa inatumika vibaya.

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa hivi tumesimamisha utoaji wa ruzuku hiyo, sasa tunaangalia namna bora ya kuwawezesha wachimbaji wadogo ambapo tukiwapa fedha zile, basi waweze kununua vifaa, wafanye tafiti mbalimbali na kuwawezesha kuchimba. hapo awali, walikuwa wanapewa hata wasiyokuwa na sifa, na kweli mpaka sasa tunafuatilia na kuhakikisha kwamba tunakwenda kuwasaidia wachimbaji wadogo tunapokuja na modality nzuri.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itafanya utafiti wa uhakika katika Vijiji vyote vya Jimbo la Morogoro Kusini ili kubaini madini yaliyopo? (b) Je, Serikali itawasaidiaje Wachimbaji wadogo wa Rubi, Spinel na Dhahabu ili waweze kuzalisha zaidi na kupata masoko ya uhakika? (c) Je, ni lini Serikali itatuma Wataalam wa kuthibitisha wingi wa madini ya Graphite na Chokaa katika maeneo ya Jimbo la Morogoro Kusini ili mipango ya kuchimba iweze kuanza?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kuna tatizo kubwa upande wa watumishi wa Madini na TMA. Kumekuwa na ucheleweshwaji sana wa ushushaji wa mashine upande wa elution na kusababisha hasara kwa wenye elution na pia kwa wachimbaji:-

Je, Serikali imejipanga vipi kuongeza watumishi upande wa TMA na Madini ili ushushaji wa mashine zile za elution iwe wa kila siku ili kupunguza zile hasara wanazozipata watu wenye elution?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli tuna tatizo kidogo kwa wafanyakazi ambao wapo katika Tume ya Madini. Kwa sababu baada ya mabadiliko ya Sheria TMA ilikufa, imeanzishwa Tume ya Madini. Kwa hiyo, sasa hivi wafanyakazi wote, walioko Mikoani wako chini ya Tume ya Madini. Tuna tatizo kidogo kwa wafanyakazi, lakini sasa hivi tuna kwenda kuongeza wafanyakazi wengi zaidi ili waweze kutoa huduma kwenye zile elution.

Mheshimiwa Spika, bado naendelea kusisitiza, watu wote wenye elution tumeona kuna matatizo makubwa sana yanayofanyika, watu wengine wanaenda kule wanafanya mambo ambayo hayaeleweki. Tunaendelea kudhibiti na tunaendelea kutoa tamko kwamba wanapo-load carbon kushusha dhahabu wasijaribu kushusha bila uwepo wa wafanyakazi wa Tume ya Madini. Tunakwenda kuongeza, lakini sasa hivi tunajitahidi kuhakikisha kwamba kila siku waendelee kutoa huduma hiyo.

Mheshimiwa Spika, namhakikishia tu Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi, tunaendelea kurekebisha.