Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 104 2023-11-07

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza:-

Je, maombi mangapi ya usajili wa Taasisi na Madhehebu ya Dini yamewasilishwa tangu 2016 na hazijapatiwa usajili na sababu za kutosajiliwa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha kuanzia mwaka 2016 hadi Septemba, 2023, jumla ya maombi ya Usajili wa Taasisi na Madhehebu ya Dini 1,858 yalipokelewa katika Ofisi ya Msajili wa Jumuiya. Kati ya maombi yaliyopokelewa, Taasisi na Madhehebu ya Dini 419 yamesajiliwa, maombi manne yamekataliwa na maombi 1,435 yapo katika hatua mbalimbali za usajili. Sababu zinazosababisha baadhi ya Taasisi na Madhehebu ya Dini kuchukua muda mrefu kusajiliwa au kotosajiliwa ni pamoja na baadhi ya Taasisi na Madhehebu ya Dini kukosa vigezo vya kusajiliwa, kubadili anwani za Posta au Makao Makuu ya Taasisi bila kutoa taarifa na hivyo kukosekana kwa mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, baadhi ya Taasisi na Madhehebu kukosa maeneo stahiki ya kuendeshea shughuli zao na kuingia katika migogoro ya ndani, migogoro na jamii inayozunguka taasisi hizo au Mamlaka za Serikali zilizopo katika maeneo hayo au kukabiliwa na kesi katika mamlaka za utoaji haki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Ofisi ya Msajili wa Jumuiya, inaendelea kushughulikia maombi ya Usajili wa Taasisi na Madhehebu ya Dini na kutoa usajili kwa wakati kwa taasisi zenye sifa stahiki na kuhakikisha kuwa Serikali haisajili taasisi na Madhehebu ya Dini ambayo yanaweza kuleta madhara kwa jamii au kuhamasisha vitendo ambavyo ni kinyume cha mila, desturi, utamaduni na maadili ya Kitanzania, nashukuru.