Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 101 2023-11-07

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Mahakama za Mwanzo katika Tarafa za Bwakira, Mvuli na Matombo – Morogoro Vijijini?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu sasa swali la Mheshimiwa Innocent Edward Kalogeris, Mbunge wa Morogoro Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mpango na Bajeti ya mwaka 2023/2024, Mahakama ya Mwanzo katika Tarafa ya Bwakira, Kata ya Bwakira Chini itajengwa ili kuwawezesha wananchi katika maeneo hayo kupata haki kwa wakati. Tayari zabuni imetangazwa kwa ajili ya kumpata mkandarasi wa ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Mahakama za Mwanzo; Matombo na Mvuha, majengo yaliyopo ni chakavu sana na hivyo kuhitaji ujenzi mpya. Hata hivyo, kutokana na mahitaji makubwa yaliyopo katika maeneo mbalimbali, ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Matombo na Mvuha utazingatiwa kwenye Mpango ujao wa ujenzi wa Mahakama, ahsante.