Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 96 2023-11-07

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: -

Je, lini ujenzi wa Vibanda vya Wajasiriamali pembezoni mwa Barabara ya Njia Nane Kimara hadi Kiluvya utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS,) imekamilisha Usanifu wa Vibanda 950 vya Wajasiliamali vitakavyojengwa pembezoni mwa Barabara ya Morogoro kuanzia Kimara hadi Kiluvya. Zabuni ziko katika hatua ya uchambuzi (evaluation) na ujenzi unatarajiwa kuanza Mwezi Desemba, 2023 na utekelezaji wake unakadiriwa kuchukua muda wa miezi sita, ahsante.