Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 90 2023-11-07

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:-

Je, kuna Mkakati gani wa Kujenga Viwanda Maalum na Maghala ya ubaridi kwenye eneo la Tanganyika Packers Mbalizi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mipango na Uwekezaji, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la Tanganyika Packers Mbalizi Shamba Na. 761 la kulishia mifugo la Nsalala lenye ukubwa ekari 4,900, Serikali imeshafanya maamuzi ya kulikabidhi eneo hilo kwa Mamlaka ya Maeneo Maalum kwa Mauzo Nje (EPZA) kwa ajili ya uwekezaji. Baada ya makabidhiano, eneo hilo litatumika kwa ajili ya uwekezaji ikiwa ni pamoja na ujenzi wa viwanda mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imechukua maoni ya Mheshimiwa Mbunge ya ujenzi wa viwanda maalum na maghala ya ubaridi katika eneo hilo na itayafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.