Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 124 2024-02-07

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kusamehe gharama za matibabu kwa marehemu ili kupunguza maumivu kwa wafiwa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Muharami Shabani Mkenge, Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilishatoa maelekezo kwa vituo vyote vya kutolea huduma za afya nchini kupitia Waraka Na. 1 wa 2021, wa kutozuia maiti na kuweka utaratibu wa kulipia gharama za matibabu na madeni ya miili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa Waganga Wakuu wa Mikoa, Waganga Wakuu wa Wilaya pamoja na Waganga Wafawidhi wa hospitali kwa ngazi zote nchini, kuzingatia maelekezo ya mwongozo huu na kuhakikisha wananchi wanapata huduma pasipo kuwepo kwa vikwazo vya kuchelewesha marehemu kuzikwa.