Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakifanyia matengenezo Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Micheweni na ujenzi wa nyumba za askari?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Serikali ingawa hayaleti matumaini kwa wananchi wa Wilaya ya Micheweni, lakini nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kulingana na hali ya kituo kilivyo hali ni mbaya sana mpaka paa zake kuvunja. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka na wa dharura kukarabati Kituo hiki cha Micheweni?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari baada ya Bunge hili kuambatana na mimi mpaka Micheweni kwenda kujionea hali halisi ilivyo kwa sababu hanga hili la polisi limejengwa kwa nguvu za wananchi takribani miaka minane iliyopita na sasa hivi tayari limeanza kuvuja. Je, uko tayari kuambatana na mimi kwenda kujionea hali halisi ilivyo? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kombo kama ifuatavyo:-

Kwanza nakubaliana naye kwamba hali ni mbaya ndiyo maana tathmini yetu imefanyika na kubaini gharama zinazohitajika. Kwa kuwa bajeti ya mwaka huu imepita, naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba katika maeneo yatakayopewa vipaumbele katika mwaka ujao basi tutazingatia hili eneo pia la Micheweni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu umuhimu wa kuambatana naye niko tayari na mara nyingi natekeleza ahadi baada ya Bunge hili tutapanga tuone lini kuweza kuitembelea Micheweni kubaini kiwango cha uharibifu na nakubaliana naye pamoja namna ya kutekeleza ukarabati huo, nakushukuru.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakifanyia matengenezo Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Micheweni na ujenzi wa nyumba za askari?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Polisi cha Tukuyu hakina uzio kwa ajili ya usalama wa kituo kile kwa sababu inazungukwa pia na shule ya msingi. Ni lini Serikali itapeleka pesa katika kituo kile ili tuweze kujengewa uzio kwa usalama wa wananchi wanaozunguka?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kupanga ni kuchagua, tumesema sasa hivi baadhi ya vituo ni chakavu sana, vinahitaji ukarabati na kwingine kunahitaji kujenga kabisa. Kwa hiyo, swali la Mbunge ni zuri kweli tunahitaji uzio, lakini kwa vipaumbele tulivyoweka uzio itakuwa ni second priority tutaanza kwanza na ukarabati hatimaye uzio utafuata, nashukuru.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakifanyia matengenezo Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Micheweni na ujenzi wa nyumba za askari?

Supplementary Question 3

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kituo cha Polisi Masumbwe kiko kwenye eneo la CCM na tumeshachukua eneo kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi pale Mbogwe. Je, Serikali inatusaidiaje Mbogwe ili kusudi askari wapate mahala pa kukaa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mbunge kwa mahusiano mema na Chama Tawala, Chama cha Mapinduzi ambao waliweza kutoa jengo linalotumika na Kituo hicho cha Polisi. Hata hivyo kama tulivyokwishasema kwenye majibu yetu ya msingi mbalimbali ni kwamba kipaumbele ni kujenga vituo vya polisi kwenye maeneo ambayo hayana kabisa, Mbogwe ikiwa ni mojawapo tutaipa kipaumbele katika miaka ijayo ili kuweza kujengea kituo chake cha polisi. (Makofi)