Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA K.n.y MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na changamoto ya uhaba wa walimu, madarasa, samani na miundombinu mingine inayochagizwa na utekelezaji wa Sera ya Elimu bila Malipo?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, katika Jimbo la Manyoni Mashariki kuna Kata ya Makutupora ambayo ilipangiwa kujenga shule mpya, lakini mpaka sasa hivi fedha ya kujenga shule mpya katika Kata ya Makutupora haijapelekwa. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka fedha hii ili shule ianze kujengwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa utoaji wa elimu ya awali katika Mkoa wa Singida bado ni hafifu; je, nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba sasa tunaajiri walimu wa elimu ya awali hususani katika maeneo ya vijijini ya Mkoa wa Singida? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Chaya, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki kama ifuatavyo;-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi ya Serikali na ujenzi wa shule ya sekondari katika Kata ya Makutupora iko pale pale na tutajenga kata hiyo kwa sababu fedha zipo katika bajeti yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili kuajiri walimu wa awali katika ajira hizi zilizotangazwa moja ya kigezo ambacho tumezingatia ni kuajiri walimu wapya ambao wana shahada ya elimu ya awali na stashahada ambao tutawapeleka katika shule zote nchini ili kusaidia hii elimu ya awali nchini.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA K.n.y MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na changamoto ya uhaba wa walimu, madarasa, samani na miundombinu mingine inayochagizwa na utekelezaji wa Sera ya Elimu bila Malipo?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na uhaba mkubwa wa watumishi katika Wilaya ya Liwale, lakini hata hivyo mgao tunapata watumishi, lakini idadi ya watumishi wanaohama na wanaohamia kubwa ni ile ambayo wanahama bila kufanyiwa replacement. Je, nini kauli ya Serikali juu ya kuhamisha watumishi bila kutupatia replacement kuziba nafasi hizo? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale, kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunatambua changamoto za maeneo ya pembezoni walimu wengi wanaoajiriwa huwa wanapenda kuhama na sasa hivi mkakati wa Serikali ni kwamba watu wote ambao tunawaajiri tunawapa na ile barua kwa maana ya commitment letter ambayo itawafanya wakae maeneo siyo chini ya miaka mitatu mpaka watakavyoomba kuhama. Lengo la Serikali ni kuhakikisha maeneo yote nchini yanakuwa na usawa wa walimu wote ambao tunawaajiri, ahsante.