Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza:- Je, Serikali haioni haja ya kuongeza kiwango cha mikopo ya vikundi vya watu watano inayotolewa na Halmashauri kutoka shilingi milioni moja hadi shilingi milioni tano?

Supplementary Question 1

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kwa fedha hizi ni revolving funds lakini bahati mbaya sana baadhi ya vikundi vinashindwa kufanya mrejesho. Je, Serikali inawachukulia hatua gani vikundi ambavyo vinashindwa kufanya mrejesho ili vikundi vingine vipate mikopo?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa biashara nyingi zilizoanzishwa na vikundi hivi vina-fail. Je, Serikali haioni haja sasa ya kufanya uchambuzi wa kina na ushauri kabla hawajatoa mikopo katika vikundi hivyo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Regina Ndege Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba wale wote ambao hawalipi mikopo kuna hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa katika kila Halmashauri, ikiwemo kuwafuata, kuwaelimisha, lakini vilevile wale ambao wamekuwa wagumu kesi zao za madai zimekuwa zikipelekwa mpaka mahakamani na wengine wamekuwa wakilipa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunaandaa mpango ambao utafanya sasa watu wote wanaokopa waweze kulipa kwa wakati ili fedha zile ziwasaidie na watu wengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, tumepokea ushauri na sasa hivi tunajaribisha kuwapa elimu Maafisa Maendeleo wa Jamii ili waweze kufanya uchamuzi wa kina pamoja na ushauri sahihi wa wale wote wanaokop ili mikopo hii iwe na tija. Ahsante.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza:- Je, Serikali haioni haja ya kuongeza kiwango cha mikopo ya vikundi vya watu watano inayotolewa na Halmashauri kutoka shilingi milioni moja hadi shilingi milioni tano?

Supplementary Question 2

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, kwa kuwa mikopo hii mara inapotolewa wakopaji uanza kulipa mara moja, lakini wapo wakulima wa mazao ya muda mrefu kama parachichi na mazao mengine yanayochukua muda mrefu.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kutoa kipindi cha kusubiria yaani grace period kabla hawajaanza? Uko tayari kutoa agizo hilo Mheshimiwa Naibu Waziri?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nyamoga, Mbunge wa Jimbo la Kilolo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mikopo hii inaongozwa kwa kanuni na sheria iliyotungwa na Bunge. Kwa hiyo, mpaka muda huu ninapozungumza bado kanuni zinazotumika ni zile ambazo zimetungwa. Kwa hiyo, ili kuongeza grace period maana yake tunahitaji mabadiliko ya kisheria ili tuweze ku-accomadate. Kwa hiyo, Bunge lako tukufu litakavyoona wakati unafaa basi mnaweza kufanya marekebisho na sisi tutatekeleza.