Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa soko la kisasa la Kwa Sadala?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwa taarifa ambazo nimepewa taarifa hii na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, ni kwamba tayari marekebisho yao yameshafanyika na imeshawasilishwa kwenye mamlaka ya ofisi yake. Swali langu, itakapofika kwenye meza yako, ni lini Serikali itaanza ujenzi huo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa soko hili likikamilika litahitaji sana mizigo mingi kutoka pembezoni kwenye maeneo mbalimbali na kata mbalimbali. Serikali ina mpango gani sasa wa kutekeleza ahadi ya Rais kwa kujenga barabara ya Shilinjoro - Mijengweni, Arusha Road – Ngalawa; na barabara ya Jiweni – Lukan - Losaa - Nakyungu? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Hai ambayo tulikuwa tumeiadikia kufanya marekebisho, wapo kwenye hatua na kwa maelezo ya Mheshimiwa Mbunge ni kama wamekabidhi. Ninachoweza kumhakikishia ni kwamba Serikali ya Awamu ya Sita, itakapopata andiko hilo maana yake tutaanza mara moja kutafuta fedha ili sasa tutekeleze ahadi ambayo ipo ya kujenga soko hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini baada ya kukamilika kwa soko maana yake tutafuta fedha zaidi sasa kurekebisho hizo barabara ambazo zinaelekea katika eneo la soko ili kurahisisha uchumi wa wananchi wa Hai. Kwa hiyo, hicho ndicho nachoweza kusema ahadi ya Serikali ya Awamu ya Sita.