Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja katika Mto Loya?

Supplementary Question 1

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nikiri wazi kweli wataalam wako katika Kata ya Loya, wanafanya usanifu.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika maswali yangu mawili ya nyongeza la kwanza, tarehe 17 Mei, Mheshimiwa Rais alipokuwa Mkoa wa Tabora nilimfikishia kero hii ya wananchi wa Loya na akamuagiza Waziri wa Ujenzi aweze kushughulikia daraja hilo.

Je, Serikali kupitia Wizara ya TAMISEMI, hamuoni kuharakisha huo usanifu ili mpeleke Wizara ya Ujenzi ili muweze kusaidia kujenga daraja hili?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili, kwa kuwa daraja hili litachukua muda mrefu kukamilika na wananchi wanaendelea kupoteza maisha, hamuwezi kuona uharaka kwa kujenga daraja la watembea kwa miguu ili wananchi wasiendelee kupoteza maisha? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Igalula kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu ambacho nina uhakika nacho ni kwamba tuko katika hatua za mwisho za kukamilisha usanifu ambao mpaka sasa hivi tumebakiza kama wiki tatu tu kukamilika. Kwa hiyo, mara baada ya kukamilika basi tutakabidhi kwa wataalam kwa ajili ya hizo fedha ili sasa zipatikane na ujenzi wa daraja uanze. Kwa hiyo, uharaka wa kujenga daraja la miguu kwa sababu hizi kazi zinaenda sambamba, nimhakikishie tu kwamba tutafanya haya yote kwa pamoja kuhakikisha kwamba wananchi wale wanapata huduma, ahsante.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja katika Mto Loya?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona daraja la Zihi – Mlambalasi kwenda Kiwele ambalo ni Jimbo la Kalenga ni daraja ambalo ni muhimu sana linatakiwa lijengwe kwa sababu linakwenda kwenye makumbusho ya Mkwawa.

Ni lini Serikali italijenga daraja hilo kwa sababu sasa hivi watu wanapita tu, ni kasehemu kadogo wanapita kwa pikipiki tu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunajenga madaraja ambayo yamekuwa sumbufu katika maeneo mbalimbali nchini. Kwa hiyo, niwaagize tu Mkandarasi wa TARURA Mkoa wa Iringa waweze kwenda kufanya tathmini na baada ya tathmini tutafute fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo. Ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja katika Mto Loya?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi, Mto Bubu umekata katikati kati ya Kijiji cha Mpendo - Hamia na hivyo kipindi cha mvua kuna na ugumu sana wa kupata mawasiliano ya barabara kuja Dodoma.

Nini mkakati wa Serikali walau wa kujenga daraja la muda ili watu wapate mawasiliano? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monni, Mbunge wa Chemba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tumelipokea ombi la Mheshimiwa Mbunge na tutatuma wataalam wetu waende wakafanye tathmnini waone ni namna gani linaweza likatekelezeka ndani ya muda mfupi. Ahsante.