Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, ni lini barabara inayotoka Karagwe kupitia Nkwenda hadi Murongo itatengenezwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mheshimiwa Waziri amenijibu mchakato. Najua na ninatambua taratibu kwamba lazima hiyo michakato ifanyike. Sasa swali langu linabaki, ni lini? Kwa sababu natambua mtatangaza zabuni na Serikali inafuata utaratibu na schedule; kwa hiyo, nataka kujua ni lini? Hilo ni swali la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: Wilaya ya Kyerwa, TANROADS ina mtandao mdogo wa barabara ya Kyerwa na TARURA wana mzigo mkubwa ikiwepo na madaraja: Je, Serikali haioni ni wakati muhimu wa kutanua mtandao wa barabara kuunganisha Kata ya Nkwenda - Songambele pamoja na Karagwe na Rwanda kwa upande wa Kusini? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY KASEKENYA MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi, huu tena siyo mchakato, tumetaja tarehe 10 mwezi huu wa Tano, zabuni imefunguliwa. Ukishafungua zabuni, maana yake tayari unaanza kujenga utakapokuwa umempitisha Mkandarasi baada ya kufanya evaluation.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili, zipo taratibu ambazo zinafuatwa ili barabara zipandishwe kutoka hadhi ya kuhudumiwa na TARURA na kuhudumiwa na TANROADS. Kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Mbunge kwamba viko vikao ambavyo vinapitia, zinaletwa kwenye Wizara, Wizara inaenda kufanya tathmini na kuona hizi barabara zinakidhi vigezo halafu zinapandishwa kutoka TARURA kuja TANROADS? Ahsante. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, ni lini barabara inayotoka Karagwe kupitia Nkwenda hadi Murongo itatengenezwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali lini itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Kibada, Kisarawe II mpaka Tundi- Songani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY KASEKENYA MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Mariam Kisangi Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti iliyopitisha jana barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami na iko kwenye manunuzi na tutajenga kilomita 41 kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, ni lini barabara inayotoka Karagwe kupitia Nkwenda hadi Murongo itatengenezwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ANTHONY A. MWANTONA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini barabara inayoanzia KK Kata ya Kimo ikipitia Ikwenjola, Ikuti, Ibungu mpaka Kafwafwa ambayo iko kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY KASEKENYA MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantona Mbunge wa Rungwe Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kutoka Kimo, Kafwafwa, Luswiswi, Katengele hadi Ibunge kwenye bajeti ya mwaka huu tunaokwenda kuitekeleza imepangwa ifanyiwe upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwa na maandalizi ya kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami baada ya kukamilisha hizo taratibu za awali, ahsante.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, ni lini barabara inayotoka Karagwe kupitia Nkwenda hadi Murongo itatengenezwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, kwa kipindi kirefu kumekuwa na mchakato wa upanuzi wa barabara ya New Bagamoyo Road na Old Baganoyo Road kwa ajili ya kuondoa foleni Mkoa wa Dar es Salaam. Na kwenye New Bagamoyo Road hususan kutoka Tegeta Kibaoni kwenda mpaka Daraja la Bagamoyo. Na kwa Old Bagamoyo Road kutoka Morocco mpaka Afrikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilitaka nijue ni lini mchakato huu utaanza kwa sababu imekuwa kwenye mipango muda mrefu na utekelezaji umekuwa finyu. Ni lini barabara hizi mbili zitapanuliwa New Bagamoyo Road kwenye eneo ambalo nimekutajia na Old Bagamoyo Road katika Ukanda wa Morocco Daraja la Mlalakua mpaka Afrikana?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY KASEKENYA MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Halima Mdee Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna mpango kabambe wa kupunguza misongamano kwenye miji na ikiwepo Mji wa Dar es Salaam. Kwa hiyo, katika bajeti tunazoenda nazo barabara hizi zimeainishwa kwamba itakuwa ni barabara ambazo zitapewa kipaumbele ili kujengwa kwa barabara nne ama sita ili kupunguza msongamano. Kwa hiyo, nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu zipo zinaendelea na fedha itakapopatikana basi hiyo kazi itaanza mara moja.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, ni lini barabara inayotoka Karagwe kupitia Nkwenda hadi Murongo itatengenezwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ni lini Serikali itapasua na kumalizia barabara inayotoka Mtowisa, Ngongo mpaka Kristo Mfalme Sumbawanga DC? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY KASEKENYA MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata Mbunge wa Viti Maalum Rukwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja pia ni ahadi ya viongozi wa kitaifa. Naomba nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatafuta fedha ili kuweza kuipasua hii barabara inayoanzia Mtowisa kama ambavyo viongozi waliahidi kufanya hivyo, ahsante.