Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je Serikali ina mpango gani wa kuunganisha barabara Kata za Ulaya, Kisanga, Malolo na Uleling’ombe katika Jimbo la Mikumi?

Supplementary Question 1

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Lazaro Londo, inaonekana fedha ambayo imetengwa kwa ajili ya barabara hiyo haitoshi. Sasa ni nini comment ya Serikali kuhakikisha kwamba barabara hiyo inatengewa fedha za kutosha ili iweze kujengwa na kukamilika na wananchi waitumie?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, barabara hii ya Kisanga, Malolo na Uleling’ombe ni barabara ambayo inatumika kama barabara mbadala kipindi barabara ya kwenda Iringa ya lami inapokuwa ina hitilafu. Je, nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba barabara hii inatengenezwa na inatumika kipindi chote cha mwaka? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. NDUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo yaliyoulizwa na Mheshimiwa Florent Kyombo kwa niaba yake, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tumetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii lakini fedha haitoshi. Kimsingi tunafahamu kwamba safari ni hatua, tunaanza na hatua moja tunakwenda na hatua nyingine, angalau Serikali imeanza kuweka fedha, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendelea kutafuta fedha kukamilisha barabara hiyo.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na hii barabara nyingine ambayo inaunganisha maeneo haya muhimu ya Kata hizi mbili ya Kisanga na Uleling’ombe nayo iko kwenye mpango. Nimeeleza hapa na tutahakikisha kwamba tunaendelea kutafuta fedha kujenga barabara hizi kadri ya upatikanaji huo. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je Serikali ina mpango gani wa kuunganisha barabara Kata za Ulaya, Kisanga, Malolo na Uleling’ombe katika Jimbo la Mikumi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kufuatia swali la msingi, Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Kilosa – Lumuma ambayo ni barabara muhimu kwa kuchukua vitunguu, iweze kupitika mwaka mzima bila ya matatizo?

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali Mheshimwia Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya barabara muhimu zote katika halmashauri zetu zote kote nchini na tumewaelekeza mameneja wa TARURA katika wilaya hizo kuweka kipaumbele kwenye barabara zote muhimu kama ambayo hii ameitaja Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma. Kwa hiyo, nitoe maelekezo kwa meneja wa TARURA wa Wilaya hii ya Kilosa lakini pia wa Mkoa wa Morogoro kuhakikisha wanaipa kipaumbele barabara hii katika bajeti ili iweze kutimiza malengo ya kusafirisha bidhaa muhimu ambazo Mheshimiwa Mbunge amesema, ahsante.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je Serikali ina mpango gani wa kuunganisha barabara Kata za Ulaya, Kisanga, Malolo na Uleling’ombe katika Jimbo la Mikumi?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa barabara nyingi za ndani za TARURA ndani ya Jimbo la Kibamba zimeharibika sana na wananchi wanashindwa kufanya shughuli zao za maendeleo; je, ni upi mkakati wa Serikali kwenye kujenga barabara ya King’ong’o – Temboni - Saranga – Ukombozi - Goba – Majengo - Kwandogo – Kwashija na Luguluni – Mbokomu? Upi mkakati wa Serikali wa kukamilisha barabara hizi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtemvu, Mbunge wa Jimbo la Kibamba kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara nyingi za Jimbo la Kibamba zina hali mbaya na sisi kwenye bajeti ya TARURA ya mwaka ujao wa fedha tumeweka kipaumbele na bajeti imeongezeka sana ya Jimbo la Kibamba na namuelekeza pia Meneja wa Manispaa ya Ubungo kuhakikisha anazipa kipaumbele barabara za Jimbo la Kibamba ili ziweze kujengwa na kuhakikisha wananchi wanapata ahueni ya kupita katika barabara ambazo ziko bora, ahsante sana.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je Serikali ina mpango gani wa kuunganisha barabara Kata za Ulaya, Kisanga, Malolo na Uleling’ombe katika Jimbo la Mikumi?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuunganisha kata zilizoko Mashariki na Kaskazini mwa Mlima Meru kwa kujenga barabara itakayounganisha barabara kuu ya Moshi na barabara kuu inayokwenda Namanga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara hizi ambazo zinaunganisha Kata za Mashariki ya Meru na Moshi na maeneo mengine yote ni miongoni mwa barabara ambazo Serikali imeweka mpango, kwanza wa kuziainisha, kuzifanyia upembuzi yakinifu, lakini kutenga bajeti kwa ajili ya kuanza ujenzi wa ukamilishaji wa barabara hizo. Lakini jambo la msingi hapa Mheshimiwa Mbunge kushirikiana na Meneja wa TARURA katika Halmashauri hii ya Arusha wafanye tathmini ya barabara muhimu zaidi ambazo zinatakiwa kupewa kipaumbele ili Serikali itenge fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hizo, ahsante.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je Serikali ina mpango gani wa kuunganisha barabara Kata za Ulaya, Kisanga, Malolo na Uleling’ombe katika Jimbo la Mikumi?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Swali langu ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga barabara kutoka Mji Mdogo wa Himo kupitia Sokoni kwenda Lotimu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Charles Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara hii ya Mji Mdogo wa Himo ambayo inakwenda kuunganisha na miji mingine ni barabara muhimu na ni barabara ambayo tulishaelekeza Meneja wa TARURA wa Mkoa wa Kilimanjaro na Meneja wa TARURA wa Halmashauri ya Moshi kuhakikisha kwamba wanazifanyia tathmini na kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi ili Serikali itafute fedha kujenga barabara hizo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tuwahakikishie kwamba tutaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya barabara hizo, ahsante.