Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji mserereko wa Kiburubutu Ifakara utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKAR D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Ukizingatia majibu mazuri ya Serikali ni kwamba tumebakiwa takribani na mwezi mmoja mpaka kufikia mwisho wa mwaka wa Serikali.

Swali la kwanza je, ni lini tutaenda kusaini mkataba huo kwa ajili ya kuanza mradi huo wa miji 28 wa Kiburubutu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili je, Serikali itakuwa tayari kwenda kusainia mikataba ya miradi ya miji 28 site maeneo ya matukio ilikuwathibitishia wananchi wa Jimbo la Kilombero kuwa Serikali ya CCM inaendelea kuupiga mwingi sana?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante; naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abubakari kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, wakati wowote mradi huu utakwenda kusainiwa kwa umuhimu wake na heshima kubwa na kazi kubwa aliyoifanya Mheshimiwa Rais wa kuhakikisha mradi huu sasa unaenda kwenye utekelezaji wakati wowote Mheshimiwa Rais akipata nafasi naamini tutakwenda kusaini mkataba huu kwa wingi wake.

Mheshimiwa Spika, swali lako namba mbili sasa Wizara tumejipanga tutaelekea kwenye hii miji 28 yote tutatawanyika na kila eneo husika tutasaini mkataba hapo.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji mserereko wa Kiburubutu Ifakara utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante, ningependa kuuliza kutoka katika Wilaya ya Busega. Wilaya ya Busega ina changamoto kubwa sana ya maji hasa katika Kata ya Nyaruhande, Rutubija na Ngasangu. Je, ni lini Serikali itapeleka maji safi na salama katika kata hizo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Minza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Busega binafsi nimeshfika pale na kufanya kazi kubwa sana kuhakikisha kata zote zinapata maji na katika kata hizi alizozitaja tayari tuna mpango madhubuti wa kuhakikisha maji yanawafikia wananchi yakiwa safi na salama na ya kutosha.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji mserereko wa Kiburubutu Ifakara utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa ruhusa yako naomba niishukuru Serikali mradi wa maji Namtumbo Mjini bomba jipya na chanzo kipya cha maji unaendelea vizuri. Kumbara, Litola mabomba ya chuma yamefika kwa ajili ya ukamilishaji.

Swali langu kwa kuwa Serikali ilitenga fedha kwa Mradi wa Mgombasi ambao unapita katika Kijiji cha Nangero, Mtumbati Maji na Mgombasi yenyewe mpaka sasa hivi mradi huo haujaanza katika bajeti hii. Je, ni lini mradi huo utaanza?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Namtumbo ni moja ya maeneo ambayo yamepewa kipaumbele sana kuhakikisha tatizo la maji sugu linakwenda kuisha na mradi huu ambao ameutaja na wenyewe upo katika hatua za mwisho kabisa kuanza utekelezaji. Hivyo nipende kutoa wito kwa mameneja wetu wa Mkoa wa Ruvuma kuhakikisha wanafuata taratibu na kuhakikisha mradi unaanza mara moja.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji mserereko wa Kiburubutu Ifakara utakamilika?

Supplementary Question 4

MHE. ESTER N. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji wa Bunda unaotoka Nyabehu hivi sasa hivi una takribani miaka 15; na mimi Ester Bulaya huu ni mwaka wa 12 naulizia mradi huu. Ni lini mradi huu utakamilika ili wananchi wa Bunda Mjini wapate maji katika kata zote 14 na usifike mwaka wa 13 nikiwa nauliza hili swali?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Bunda tayari tupo kazini na kama miaka 15 kazi haikufanyika basi Mama Samia fupa lililomshinda fisi linakwenda kutafunwa, tumejionea miradi ambayo imekuwa sugu na sasa hivi inatoa maji, hivyo, Bunda pia wakae mkao wa kufungua bomba na kupata maji safi na salama na kata zote 14 tunahakikisha zinakwenda kupata maji safi na salama. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji mserereko wa Kiburubutu Ifakara utakamilika?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Serikali ilitenga fedha nyingi kwaajili ya miradi ya maji kule Arumeru Mashariki mwaka huu wa fedha lakini kuna mradi ambao hatujajua hatma yake.

Je, ni lini mradi wa maji Kata ya Ibaseni, Maji ya Chai na Kikatiti utaanza kutekelezwa kwa maana ya kwamba upo kwenye miradi inayopaswa kutelezwa mwaka huu? Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge yeye mwenyewe kazi kubwa tuliyoifanya jimboni kwake, nimekwenda na tumetembelea miradi yote ambayo ilikuwa ni historia maji kufika tayari unafahamu maji yanatoka. Hivyo, katika mradi huu ulioutaja endapo mwaka huu wa fedha utaisha utekelezaji utakuwa haujakamilika mwaka ujao wa fedha ni lazima maeneo haya yote tuje tuendelee kufanyia kazi na kuhakikisha maji yanapatikana. (Makofi)

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji mserereko wa Kiburubutu Ifakara utakamilika?

Supplementary Question 6

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kata ya Kichiwa hasa vijiji vya Kichiwa, Tagamenda, Upami na maeneo mengine kuna ahadi ya muda mrefu ya kupelekea maji kwa wananchi. Je, ni lini ahadi hii ya Serikali itakwenda kutekelezwa? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, maeneo haya aliyoyataja yapo katika mipango ya Wizara katika kuhakikisha maji yanawafikia wananchi. Kata hizi tutakwenda kuzitekeleza kadri ya jiografia yake, endapo bomba kuu itachukua muda mrefu kuwafikia basi visima virefu vitahusika lengo ni kuhakikisha maji yanapatikana bombani. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji mserereko wa Kiburubutu Ifakara utakamilika?

Supplementary Question 7

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa Wizara ya Maji kupitia DAWASA inaendelea na kazi nzuri ya upanuzi wa miundombinu ya Ruvu Juu na Ruvu Chini, lakini yapo maeneo jirani na mitambo hiyo hayana maji kwa mfano; Kata ya Mzenga, Vihingo, Kisarawe.

Je, ni lini Serikali itasambaza maji kwenye kata hizo ambapo ni jirani kama kilometa 20 kutoka Mji wa Mlandizi? Ahsante sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Subira Mgalu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nipokee kwanza pongezi na kutambua kazi kubwa inayofanywa na DAWASA; maeneo haya uliyoyataja Mheshimiwa Mbunge yanaelekea kufikiwa baada ya miradi mikubwa sana ambayo inaendelea kufanyika pale DAWASA na maeneo yote ya huko ulikotaja Mzinga, Kisarawe kote yanatarajiwa kupata maji ifikapo mwaka ujao wa fedha. (Makofi)