Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Sekta ya Uvuvi hapa Tanzania inaajiri wananchi wengi lakini wavuvi hawanufaiki kutokana na changamoto mbalimbali:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupitia mlundikano wa leseni kwani kuna aina nyingi sana za leseni, kwa mfano, leseni ya chombo, leseni ya mvuvi, leseni ya aina ya samaki, leseni ya eneo la uvuvi na kadhalika? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha wavuvi nyenzo za uvuvi ili waondokane na uvuvi haramu? (c) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri, nataka kumuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali haijawekeza kikamilifu katika sekta ya uvuvi na kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amekiri kwamba kodi zinazotozwa wavuvi ni nyingi sana na zisizokuwa na mpangilio. Nataka nitolee mfano wa Mafia ambapo Wilaya hiyo imesema kwamba kila boti itakayokuwa inaingia pale inatozwa shilingi milioni tano; whether wamevua au hawajavua. Je, Serikali itakuwa tayari katika bajeti ijayo kutuletea majibu ya kina katika Finance Act kuhakikisha kwamba kodi hizi zote zimehuishwa na zile kodi ambazo ni kero kufutwa? Swali la kwanza hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika ardhi ya Kigamboni tulikuwa na taasisi inaitwa TAFICO (Tanzania Fishing Company) ina majengo na ilikuwa inafanya kazi ya uvuvi pale Kigamboni. Majengo yale yapo pale mpaka sasa hivi hayafanyi kazi yoyote. Je, Serikali itakuwa tayari kubadilisha majengo ya taasisi ile kuwa kiwanda cha kuchakata samaki ili kuongeza ajira na kuongeza thamani ya mazao ya bahari?

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, hizi kodi kama nilivyosema kwenye maswali yaliyotangulia na katika swali hili, zipo nyingi na kwa kweli Mheshimiwa Rais alikwishatoa maelekezo kwamba ni lazima zipitiwe upya na hizo ambazo zinastahili kuondolewa kwa sababu zina kero mbalimbali ziondolewe siyo kwenye mazao ya uvuvi peke yake, lakini kama nilivyosema awali hata kwenye mazao ya kilimo pia. Kwa hivyo, kodi zile ambazo zitaondolewa na zisiwe na madhara yoyote ya kibajeti baada ya ile Kamati kukamilisha kazi yake zitaondolewa na zile ambazo zitakuwa na madhara ya kibajeti hizo zitasubiri sasa utaratibu wa bajeti ya mwaka ujao wa fedha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ni wazo na mimi nalichukua, nitakwenda kuzungumza na wenzangu katika Wizara na Serikali kuona pendekezo hili la Mheshimiwa Dkt. Ndugulile linaweza kutekelezwa namna gani.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Sekta ya Uvuvi hapa Tanzania inaajiri wananchi wengi lakini wavuvi hawanufaiki kutokana na changamoto mbalimbali:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupitia mlundikano wa leseni kwani kuna aina nyingi sana za leseni, kwa mfano, leseni ya chombo, leseni ya mvuvi, leseni ya aina ya samaki, leseni ya eneo la uvuvi na kadhalika? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha wavuvi nyenzo za uvuvi ili waondokane na uvuvi haramu? (c) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY M. KEISSY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Katika Ziwa Tanganyika tuna Halmashauri tano na kila Halmashauri ina licence yake na mvuvi anakata licence, lakini anapotaka kuhama kwenda Halmashauri nyingine hata kama licence yake haijakwisha muda lazima alipie licence upya kwenye Halmashauri anayokwenda. Je, ni lini Serikali itaondoa kero hii kwa wavuvi?

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama nilivyosema hapo awali kwamba ziko tozo ambazo zimekuwa ni chanzo cha mapato ya Halmashauri mbalimbali na moja ya vyanzo hivi vya mapato kwa Halmashauri zetu ni leseni. Bahati mbaya sana kwa kanuni tulizonazo na Sheria ya Uvuvi iliyopo leseni hizi za Halmashauri zimekuwa za maeneo ya Halmashauri husika yaani hazihamishiki na ndiyo maana kumekuwa na huu usumbufu kwa wavuvi kwamba leseni zinazotolewa na Halmashauri ya Sikonge haiwezi kwenda kutumika katika Halmashauri ya Urambo, hili ndilo limekuwa changamoto. Nimpe tu faraja Mheshimiwa Mbunge kwamba hili nalo liko katika mambo ambayo yanaangaliwa na hiyo Tume ya Taifa ya Makatibu Wakuu inayopitia upya hizi kodi ambazo zimekuwa kero kwa wananchi.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Sekta ya Uvuvi hapa Tanzania inaajiri wananchi wengi lakini wavuvi hawanufaiki kutokana na changamoto mbalimbali:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupitia mlundikano wa leseni kwani kuna aina nyingi sana za leseni, kwa mfano, leseni ya chombo, leseni ya mvuvi, leseni ya aina ya samaki, leseni ya eneo la uvuvi na kadhalika? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha wavuvi nyenzo za uvuvi ili waondokane na uvuvi haramu? (c) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi?

Supplementary Question 3

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Naomba niulize swali moja tu la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa uvuvi ni kazi inayozalisha ajira hapa nchini. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga chuo ambacho kitasaidia kusomesha wavuvi tukaweza kupata tija katika nchi yetu?

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli uvuvi ni shughuli ambayo inahitaji ujuzi fulani kama ilivyo kilimo na shughuli nyingine zote za uzalishaji. Ili kupeleka maarifa kwa wananchi kwanza Serikali inavyo vyuo kadhaa vya uvuvi. Vyuo hivi vinatumika kufundisha wataalam ambao wao sasa kama Maafisa Ugani wanapelekwa katika vijiji na halmashauri zetu ili maarifa hayo waliyonayo wayafikishe kwa wavuvi mbalimbali wanaofanya shughuli hizo. Itakuwa vigumu sana wavuvi wote nchini kuwapeleka kwenye vyuo lakini Maafisa wetu wa Ugani kwa maana ya Maafisa Uvuvi katika halmashauri zetu mbalimbali wao ndiyo wanaopaswa kufikisha maarifa ya uvuvi kwa wavuvi ili waweze kuvua kwa tija.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Sekta ya Uvuvi hapa Tanzania inaajiri wananchi wengi lakini wavuvi hawanufaiki kutokana na changamoto mbalimbali:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupitia mlundikano wa leseni kwani kuna aina nyingi sana za leseni, kwa mfano, leseni ya chombo, leseni ya mvuvi, leseni ya aina ya samaki, leseni ya eneo la uvuvi na kadhalika? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha wavuvi nyenzo za uvuvi ili waondokane na uvuvi haramu? (c) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Uvuvi katika bahari na katika maziwa makubwa unafanyika usiku na mchana, lakini uvuvi katika Mto Koga kule Sikonge unafanyika mchana tu usiku Serikali inakataza. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, ni kwa nini Sikonge tu ndiko uvuvi unakatazwa usiku wakati ndiyo kuna samaki wengi? Ahsante sana.

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, Sikonge nimekaa miaka mitano kama Mkuu wa Wilaya na kwa hivyo hiki anachokisema nakifahamu vizuri sana. Ni kweli kwamba uvuvi katika mito na mto huo bahati mbaya eneo ambalo uvuvi unafanyika ni ndani ya hifadhi. Kwa hivyo, ili kuzuia shughuli ambazo si za kivuvi wakati wa usiku ndiyo maana imepigwa marufuku kufanya uvuvi usiku katika eneo hilo. Pia katika Mto huo Koga uvuvi pia unafanywa kwa msimu, wakati ule ambako shughuli za uwindaji katika hifadhi hiyo haziruhusiwi na uvuvi pia unazuiwa ili kutoa nafasi kwa samaki kuzaliana kwa ajili ya msimu unaofuata.