Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka Askari Polisi katika Kituo cha Polisi Kata ya Kilungule - Mbagala ili wananchi wa kata hiyo wapate huduma?

Supplementary Question 1

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na juhudi nzuri za Serikali za kufungua kituo hiki siku nne zilizopita, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na tishio la panya road waliojaa Dar es Salaam, Serikali haioni haja ya kituo hiki kufanya kazi masaa 24 kama jibu linavyosema, badala ya masaa nane ambayo kinafanya sasa hivi kuanzia saa tatu mpaka saa nane? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali haioni haja Kituo cha Kiburugwa kwa kata ya jirani kukikarabati ili kiendane na mazingira bora ya watumishi wa Polisi kufanyia kazi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ntate Mbunge wa Viti Maalum Dar es Salaam, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja; hili la kufanyakazi saa 24 ndiyo maagizo ya wizara na ni maagizo ambayo IGP ameyapokea na kuelekezwa kwa viongozi wa Polisi Kanda, Mkoa na Wilaya za Dar es Salaam. Kwa hiyo, nitasisitiza kwamba hili lifanyike kwasababu tayari kuna askari sita na mkaguzi mmoja ambaye ni Mkuu wa Kituo hicho hakuna sababu zozote za msingi za kufanya kazi chini ya masaa ishirini na nne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kukarabati kituo cha Kiburugwa kama alivyokwishasema Mheshimiwa Mbunge nakubaliana nae baadhi ya vituo vilivyo katika hali mbaya vinahitaji kukabaritiwa hii ni moja ya kuweka mazingira bora ya askari wetu kufanya kazi lakini pili kuwahudumia hawa ambao wanapelekwa vituo wawe katika mazingira bora zaidi. Kwa hiyo, nakubaliana na wewe Mheshimiwa tutatafuta fedha kwaajili ya kukabarati vituo vilivyochakaa kikiwemo hiki cha Kiburugwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka Askari Polisi katika Kituo cha Polisi Kata ya Kilungule - Mbagala ili wananchi wa kata hiyo wapate huduma?

Supplementary Question 2

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, swali langu ni dogo sana lakini la uhakika. Je, ni lini Serikali itakipandisha hadhi Kituo cha Polisi cha Tandika ambacho tunatumia kata kama tano kwenda pale na sasa unaona kama kuna uhalifu mkubwa sana upande ule. Je, ni lini sasa mtakipandisha hadhi hata kipate class B ili tuweze kuona kwamba kazi nzuri inafanyika? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilave kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze kwa namna anavyofuatilia masuala ya ulinzi na usalama katika Mkoa wa Dar es Salaam mara kadhaa amenisumbua kidogo kuhusu hata njia inayokwenda Mbagala kupitia eneo la polisi na tumeshakubaliana ile njia itafunguliwa Mheshimiwa Mbunge lakini kuhusu ili la kupandisha hadhi kwa kupitia Bunge lako Tukufu namuelekeza Kamishna Kanda Maalum ya Dar es Salaam na Uongozi wa Polisi wa Mikoa ya Kipolisi Dar es Salaam kufuatilia, kupima na kufanya tathimini ya mahitaji ya kupandisha hadhi kituo hiki kama sababu alizozisema Mheshimiwa Mbunge zipo basi waone uwezekano wa kukipandisha ili kikidhi mahitaji ya eneo la Tandika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka Askari Polisi katika Kituo cha Polisi Kata ya Kilungule - Mbagala ili wananchi wa kata hiyo wapate huduma?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Vituo vya Polisi vidogo yaani kwamaana ya outpost nyingi zimechakaa sana zina hali mbaya nyingi zinavuja mapaa mbao zimeoza yaani hata hao mapolisi wanaofanyakazi huko vijijini Mungu anawalinda. Ningetaka kujua ni lini sasa Serikali itakarabati vituo hivi vidogo vyote Tanzania nzima ili viweze kuwa na hadhi ambavyo vinafaa kuwahudumia wananchi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua na nimesema kwenye majibu yangu ya msingi kwamba tunatambua uwepo wa uchakavu kwa baadhi ya vituo vya polisi vikiwemo hivi vituo vidogo. Katika mkakati wetu wa ujenzi na ukarabati wa maeneo haya tutazingatia pia hivi vituo vidogo vya polisi kama ambavyo tumeanza kufanya kwenye maeneo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka Askari Polisi katika Kituo cha Polisi Kata ya Kilungule - Mbagala ili wananchi wa kata hiyo wapate huduma?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Wilaya ya Liwale kijiografia imekaa vibaya sana hasa kwa ulinzi tunayoahadi ya kujengewa vituo vya polisi kwenye Tarafa ya Kibutuka, Kata ya Lilombe na Kata ya Kimambi. Nini kauli ya Serikali juu ya kutekeleza ahadi hiyo ili kuimarisha ulinzi kwenye Wilaya yetu ya Liwale? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, japo hajaniambia ahadi ilitolewa na nani lakini nikiri tu, kwanza maeneo yote ya tarafa yanahitaji kuwa na vituo vya polisi vyenye hadhi ya kutimiza majukumu ya ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao zikiwemo hizi tarafa ulizozitaja za Liwale kwa maana ya Kibutuka na tarafa hizo nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulingana na bajeti tuliyonayo tunakwenda kwa awamu. Kama tulivyokubaliana na Mheshimiwa Kuchauka tutafanya ziara Mkoa wa Lindi ili kuona uhitaji wa vituo hivi ili kuweka msukumo kwenye jeshi la polisi waweze kuvizingatia katika mipango yao ya ujenzi na ukarabati wa sekta nzima ya polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.