Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Uvinza?

Supplementary Question 1

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo hili analotolea majibu kwamba halina hati, lina kituo kidogo cha Polisi cha muda mrefu; na eneo hili halina mgogoro; sasa ni kwanini Serikali isijenge na hiyo hati ikaja kupatikana baadaye kwa sababu hakuna anayelalamikia eneo hilo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wilaya yangu ni kubwa sana na ni mpya, lakini OCD hana gari ya kufanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tumpongeze Mheshimiwa Nashon kwa ufuatiliaji wake wa karibu wa masuala ya ulinzi na usalama kwenye jimbo lake. Pia tumtie moyo kwa namna anavyoshirikiana na uongozi wa Wilaya ya Kigoma na kwa sababu tunafahamu hata hili jengo linalotumika sasa ni lile ambalo Halmashauri imetoa kuiazima Jeshi la Polisi waweze kufanya shughuli zao, kwa hiyo, tunakushukuru sana Mheshimiwa Bidyanguze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo hayo sasa nijibu swali lako kwamba kama kweli hakuna mgogoro, basi tutamwagiza OCD na RPC wa Mkoa wa Kigoma kufuatilia kwa haraka, kwa sababu maelekezo ya Serikali ni kwamba maeneo yote ya Serikali yapate hati ili kuondoa uwezekano wa migogoro huko mbele. Kwa hiyo, hati itakapokuwa imetoka na kwa sababu hati inatolewa na Halmashauri na mahusiano yenu ni mema, bila shaka wataharakisha kutoa hii hati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la gari, tumejibu hapa mara nyingi Mheshimiwa Mbunge, kwamba magari ambayo tunatarajia kuyapata ifikapo Septemba ni zaidi ya 370. Tunatarajia maeneo yenye changamoto kama hili la kwako la Kigoma ambalo liko karibu na maeneo ya mpakani yatazingatiwa kama maeneo ya kipaombele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Uvinza?

Supplementary Question 2

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Wilaya ya Rorya, ni moja ya wilaya ambayo ipo kwenye kanda maalum kwa maana ya Tarime na Rorya, lakini ni wilaya ambayo haina Kituo cha Polisi cha Kiwilaya, ina Vituo vya Polisi vya Kikanda kwa maana ya Utegi, Kinesi na Shirati. Nataka nijue mpango mkakati wa Serikali wa kujenga Kituo cha Polisi cha Wilaya nzima ya Rorya, itakuwa iko kwenye mpango kule?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chege, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunafahamu kwamba ziko wilaya nyingi hasa hizi wilaya mpya hazina vituo vya wilaya ya Polisi, ikiwemo hii Wilaya ya Rorya. Mpango wa Serikali kama ilivyosemwa wakati Waziri akiwasilisha hotuba yake hapa; tuna mkakati wa kujenga vituo vya Polisi kwenye mikoa ambao hawana vituo vya Polisi kwa ajili ya RPC na vilevile kwenye wilaya ambazo hazina Vituo Vikuu vya Polisi vya Wilaya. Kwa hiyo, mpango huo kadri tutavyokuwa tunapata fedha utaekelezwa, na Wilaya ya Rorya itakuwa ni moja ya wilaya ya vipaumbele kwa sababu iko mpakani.

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Uvinza?

Supplementary Question 3

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto inayowakabili wananchi wa Uvinza, inakwenda sambamba na Wilaya ya Kakonko. Mkuu wa Polisi wa Wilaya hana ofisi, anatumia iliyokuwa Ofisi ya Polisi ya Kata. Kwa hiyo, Waziri anaweza akaona hali halisi:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini kauli ya Serikali katika kuhakikisha kwamba Wilaya ya Kakonko nayo inapata Kituo cha Polisi? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye majibu ya msingi, wilaya zote mpya hazijawa na vituo vya Polisi vya ma-OCD. Ndiyo maana tumekuja na mkakati wa kujenga vituo hivyo kwenye maeneo ambayo hayana. Katika bajeti iliyopita tutaanza ujenzi wa vituo hivyo, lakini kipaumbele kitawekwa kwenye maeneo yaliyoko mpakani ikiwemo hii Wilaya ya Kakondo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Uvinza?

Supplementary Question 4

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Njombe, ni miaka 10 toka umeanzishwa na mpaka leo hatuna Kituo cha Polisi kinachoendana na hadhi ya mkoa? Ni lini sasa kituo hicho cha Polisi kitajengwa katika Mji wa Njombe?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwanyika, Mbunge kutoka Njombe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwishasema, tunatambua mikoa mipya iliyoanza kwenye miaka ya 2012 ukiwemo Mkoa wa Njombe, hauna kituo kikuu cha Polisi kwa maana Ofisi ya RPC. Kwa kweli Mkoa wa Njombe tayari uko kwenye mpango na Mheshimiwa Mbunge anajua. Katika vipaumbele ambavyo mwaka huu tunaendelea navyo, ni ujenzi wa ofisi ya RPC Njombe. Nadhani baada ya Bunge hili tutatembelea maeneo hayo kuona maandalizi na harakati za ujenzi zinavyoendelea Meshimiwa Mwanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Uvinza?

Supplementary Question 5

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua ni lini Serikali itakijenga kwa hadhi ya Kituo cha Polisi Mbagala?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chaurembo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli swali hili ni moja ya maswali ambayo yako kwenye mpango wa kujibiwa, lakini niseme tu kwamba tunajua Mkoa wa Dar es Salaam, ikiwemo Wilaya ya Temeke, na Majimbo ya Mbagala, na majimbo mengine ya maeneo ya Kigamboni, kuna vituo vidogo vya Polisi vingi kuliko vituo vya ngazi ya wilaya. Tunaendelea na mpango mkakati wa ujenzi wa vituo hivi kwa kuangalia maeneo ambayo yana uhitaji mkubwa kutokana matukio ya uhalifu ili kuyazingatia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naamini Mbagala kwa sababu ya wigi wake wa watu, matukio ya uhalifu pia yatakuwa mengi, tutakizingatia katika mpango huu wa ujenzi.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Uvinza?

Supplementary Question 6

MHE. JESECA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa viongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani wana afya nzuri ya akili, ni lini sasa watatujengea nyumba za askari katika Kituo Kikuu cha Polisi pale Iringa Manispaa? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashukuru Balozi wa Afya ya Akili anatambua jinsi tulivyo timamu. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi yangu ni hiyo, kwamba katika ujenzi wa vituo vya Polisi huenda sambamba na ujenzi wa nyumba za Maaskari, Wakaguzi na Maofisa. Kwa hiyo, Iringa kama alivyosema ni mjini, ukiangalia kwa vipaumbele, pale angalau watu wanaweza wakapata nyumba zenye hadhi za kupanga, lakini kuna maeneo ya vijijini kabisa ambayo uwezekano wa kupata nyumba za kupanga ni changamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwenye ujenzi wa nyumba, vipaumbele tutaweka kwenye maeneo ambayo yana changamoto kubwa za kupata makazi. Kwa hiyo, wale wa Iringa watasubiri, lakini kadri fedha zitakapopatikana na wao pia watajengewa.