Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji kutoka Ziwa Basotu kwa ajili ya Vijiji zaidi ya tisa (9) utaanza kutekelezwa Wilayani Hanang’?

Supplementary Question 1

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza maji ya Ziwa Bassotu kwa siku za karibuni yamekuwa yakisambaa na kuingia kwenye mashamba ya watu na nyumba:-

Je, Wizara ya Maji iko tayari kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, (Mazingira) kuangalia na kufanya tathmini ya tatizo linalofanya hayo maji yasambae na hatimaye kulitatua?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mradi huu karibu miaka mitatu ya fedha imekuwa ikitengewa chini ya Shilingi bilioni moja na tathmini ya awali ni Shilingi bilioni 12:-

Je, Wizara sasa iko tayari kutenga fedha zaidi ili mradi huu ukamilike kwa wakati?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Samweli Hhayuma, Mbunge wa Hanang’ kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Wizara tunafanya kazi kwa ushirikiano na Wizara ambazo tunakuwa tunaingiliana kikazo. Hivyo tupo tayari kushirikiana ili kuondoa hiyo adha kwa wananchi na vilevile kutenga fedha zaidi. Tutaendelea kufanya hivyo na pale tunapoendelea kupata fedha tutaongeza bajeti kwenye eneo hilo ili miradi hii ikamilike.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji kutoka Ziwa Basotu kwa ajili ya Vijiji zaidi ya tisa (9) utaanza kutekelezwa Wilayani Hanang’?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Umekuwepo mradi wa Kwembe-King’azi wa muda mrefu ambao uliahidiwa kukamilika mwezi wa Kumi na Mbili mwaka 2021 mbele ya Mheshimiwa Waziri na mpaka sasa haujaanza:-

Je, ni lini mradi wa Kwembe-King’azi A utaanza ili wananchi wa pale waweze kupata maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu tunaendelea katika hatua zake za mwisho kabisa na unaelekea kwenye utekelezaji.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji kutoka Ziwa Basotu kwa ajili ya Vijiji zaidi ya tisa (9) utaanza kutekelezwa Wilayani Hanang’?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kumekuwa na tatizo kubwa la Wakandarasi kushindwa kuchimba visima. Katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Mkandarasi ana miezi sita, ameshindwa kuchimba visima vya Aicho, Boboa na Titimu:-

Je, Serikali imefikisha hatua gani kuleta mitambo ya kila mkoa kuchimba visima vyetu? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Mbulu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, napenda kuendelea kumshukuru Mheshimiwa Rais, ametupatia fedha ya kutosha, taratibu zote zilishafanywa. Kabla ya mwaka huu wa fedha kwisha tunatarajia mitambo ile yote iwe imeshafika Tanzania na iweze kwenda kufanya kazi inayokusudiwa.