Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Handeni Kibirashi, Kondoa hadi Singida kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, toka mwaka jana kwenye bajeti majibu ya Serikali yamekuwa ni haya haya hayabadiliki. Hatua za mwisho za kusaini mkataba. Swali langu la msingi lilikuwa ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ipi Barabara ya Handeni - Kwa Magome, Nziha - Turiani. Ni lini Serikali pia itaanza kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Reuben Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Reuben kwa jinsi anavyofuatilia barabara ambazo zinaanzia katika Jimbo lake kwenda kwenye Majimbo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ninavyoongea nataka nimhakikishie Mheshimiwa Reuben kwamba tayari kazi ya ujenzi imeshaanza na hivi tunavyoingia huku Mkandarasi ameshapatikana na sasa ameanza mobilization kupeleka vifaa site kwa hizo kilomita 20 ambazo zilishatangazwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu barabara ya kutoka Handeni Mjini kuja Turiani naomba tusubiri bajeti ipitishwe halafu tuone tutakachofanya katika hiyo barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)