Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Uwanja wa Ndege katika Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 1

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Je, kutokana na viwanja vingi vya Serikali kujengwa na makampuni ya nje. Nini kauli ya Serikali kuwajengea uwezo makampuni ya ndani ili yaweze kujenga viwanja hivi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kutokana na mkataba huu kusainiwa tangu umesainiwa ni miaka Mitano. Nini kauli ya Serikali itawalipa fidia lini hawa wananchi wa Shinyanga kwa sababu tangu mwaka 2017 mpaka sasa 2022 miaka mitano imepita, itawalipa fidia ya mwaka 2017 au mwaka 2022, kutokana na bidhaa nyingi kupanda?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Santiel Eric Kirumba, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Shinyanga, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Mbunge Santiel kwa jinsi anavyofuatilia ujenzi wa uwanja huu. Suala la Wakandarasi wa ndani. Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imekuwa mara kwa mara ikihimiza na ikiwajengea uwezo Wakandarasi wote wa Tanzania ili waweze kufanya miradi mikubwa. Hii siyo tu kwa viwanja vya ndege ni pamoja na miundombinu mingine ikiwemo majengo makubwa na hata barabara. Kwa hiyo, kinachofanyika kwanza ni kuwapa elimu ya kuwaunganisha pamoja ili waweze kuwa na mitaji mikubwa pia kuwawezesha ili waweze kupata mikopo kwa taasisi mbalimbali za fedha ikiwemo mabenki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ipo inafanya kazi hiyo na tunaamini kwa kuwawezesha Wakandarasi wa ndani maana yake fedha yetu nyingi itaendelea kubaki na kukuza uchumi pia kuwezesha uwezo wa hawa Makandarasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu fidia. Serikali ilikwishawalipa fidia wananchi ambao wamepisha ujenzi. Kwa mujibu wa sheria zetu tunapolipa fidia tunaondoa kitu kinachoitwa uchakavu na hasa uchakavu wa majengo. Masharti ya wenzetu hawa ambao wanatoa fedha wana sharti moja kwamba ni lazima fedha ya uchakavu pia ilipwe. Kwa hiyo, Serikali imeshafanya tathmini ya uchakavu wa yale majengo na tayari yameshawasilishwa Wizara ya Fedha ili wakalipwe zile fidia za nyongeza kwa uchakavu wa yale majengo. Kwa hiyo, tayari tuko kwenye process na hawa watu wataongezwa fidia kwa maana ya ile ambayo sheria yetu ilikuwa inasema tusiwalipe lakini wanaotufadhili wanatuambia ni lazima pia walipwe. Kwa hiyo wananchi hawa watapata nyongeza ya fidia tofauti na waliyopata ile ya awali. Ahsante. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Uwanja wa Ndege katika Mkoa wa Shinyanga?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Je, Serikali itamaliza lini uwanja wetu wa ndege wa Iringa, kwa sababu uwanja ule tunategemea sasa hivi Mama amehamasisha royal tour kwa ajili ya utalii mkubwa katika hkivutio cha Ruaha na vivutio vingine vilivyoko katika Mkoa wa Iringa na Nyanda za Juu Kusini? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Iringa, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba ujenzi huu unaendelea. Serikali inaendelea kuujenga uwanja huu na Wakandarasi wako site. Pengine tu ni kuwahimiza Wakandarasi waweze kuongeza speed na tunajenga kwa fedha ya Serikali pia wenzetu wa World Bank wameonesha utayari wa kuweza kusaidia ili kukamilisha ujenzi wa uwanja huu ili kuweza kuimarisha shughuli za utalii ambazo tayari Mheshimiwa Rais ameshakuwa champion wa hiyo kazi. Kwa hiyo tunakuhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba uwanja huu tutaukamilisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.