Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha kwa ajili ya kumalizia Miradi ya Afya iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Swali la kwanza; kwa kuwa majibu ya Serikali yanaonesha kabisa fedha iliyotengwa ni ndogo kulinganisha na miradi ya wananchi. Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya kuongeza fedha ili kuweza kumalizia miradi ambayo nguvu za wananchi zimetumika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa kuona miradi hiyo ama nguvu hizo za wananchi kwa kuanzia tuanze na Mkoa wa Manyara?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Asia Abdukarimu Halamga Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunatambua kwamba wananchi wamefanya kazi kubwa sana ya ujenzi wa maboma na fedha ambayo tumetenga bado haikidhi, lakini Serikali inaendelea kutafuta fedha kuhakikisha kwamba tunakamilisha na kuongeza jitihada ambazo wananchi wamezifanya. Kwa hiyo nimwondoe shaka kwamba, tutaendelea kuongeza kwa mfano mwaka huu na mwakani mwaka wa fedha unaofuatia, Serikali itaongeza fedha ili kuhakikisha maboma hayo yanakamilishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, niko tayari kwenda kujionea hiyo miradi Mkoa wa Manyara nikiongozana na Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum pamoja na Wabunge wote wa Mkoa wa Manyara. Ahsante sana.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha kwa ajili ya kumalizia Miradi ya Afya iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kumalizia zahanati na kuna baadhi ya zahanati ambazo tumeshakamilisha katika Wilaya ya Nyangh’wale. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kupeleka vifaa tiba na kuweza kuzifungua zahanati hizo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Nassoro Amar, Mbunge wa Nyangh’wale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna maeneo mengi ambayo mpaka sasa wameshamaliza vituo vya afya pamoja na zahanati. Sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tumeshafanya uagizaji wa vifaa tiba na baadhi ya tender zipo katika hatua za mwisho kwa ajili ya kuagiza hivyo vifaa. Kwa hiyo mara vifaa hivyo vitakapofika basi tutapeleka katika vile vituo ambavyo vimekamilika ili kuhakikisha kwamba zahanati hizo pamoja na vituo vya afya vinafunguliwa. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha kwa ajili ya kumalizia Miradi ya Afya iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itamalizia Hospitali ya Wilaya Sumbawanga Mjini inayoitwa Isyofu, ambayo bado wodi hazijaisha. Ni lini sasa Serikali itapeleka fedha ili wodi zijengwe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hospitali ya Sumbawanga Mjini nilifika mimi mwenyewe pale na nilijionea adha ambayo inaendelea pale na najua bado haijakamilika. Commitment ya Serikali ni kuhakikisha kwamba tunatafuta fedha ili tuongezee na kuikamilisha ile hospitali kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha kwa ajili ya kumalizia Miradi ya Afya iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Halmashauri wa Mji wa Mafinga Kata ya Bumilainga kwa kufuata maelekezo ya Serikali kwamba tutenge fedha za mapato ya ndani kujenga kituo cha afya, tumetekeleza na tuko kwenye hatua za mwisho za kukamilisha Kituo cha Afya cha Bumilainga. Je, Serikali mpo tayari kutuletea vifaa ili kituo hichi cha afya kianze kazi, ambacho kinahudumia pia Halmashauri ya Mufindi anakotoka Mheshimiwa Mwenyekiti?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mhheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Cosato Chumi Mbunge wa Mafinga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu kwamba mara baada ya kituo hicho cha afya kukamilika tupo tayari kupeleka vifaatiba pamoja na Wauguzi ili kiweze kufunguliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)