Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara za mitaa ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa kwa kiwango cha lami kupitia Miradi ya TACTIC?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanz; Mji wa Kondoa Mjini una hali mbaya sana hasa kipindi cha mvua kwa kuwa na mafuriko katikati ya mji. Je, Serikali inaweza ikatupa fedha kwa ajili ya kujenga mitaro kuzuia yale mafuriko kutokea mitaa ya Uwanja wa Puma mpaka katikati ya mji?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; tuna barabara ya kilomita kama moja kutoka barabara kuu kwenda katika Ofisi za Mkurugenzi maana yake majengo ya halmashauri . Je, Serikali ipo tayari kusaidia fedha kwa ajili ya kuweka lami kwa sababu ya ule muundombinu uliowekwa pale, jengo zuri la thamani kubwa lakini barabara ya tope?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Juma Makoa, Mbunge wa Jimbo la Kondoa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba katika bajeti ambayo tumepitisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI, sehemu ya fedha ambazo tumeziweka ni pamoja na Jimbo la Kondoa na sehemu ya fedha hiyo itahusika katika ujenzi wa mitaro ambayo Mheshimiwa Mbunge ameainisha. Kwa hiyo nimwondoe shaka tu kwamba kwa kuwa tumeshapitisha bajeti, basi tutakwenda kutekeleza kama ambavyo yeye amehitaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuhusiana na mahitaji ya kilomita moja kutoka barabara kuu ya lami kwenda katika jengo lao la halmashauri, niseme tu ombi hili tumelipokea japo tunatambua kwamba Mradi wa TACTIC sehemu mojawapo ni kutekeleza mradi huu ambao Mheshimiwa Mbunge ameainisha. Ahsante.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara za mitaa ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa kwa kiwango cha lami kupitia Miradi ya TACTIC?

Supplementary Question 2

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Serikali kupitia Halmashauri ya Manispaa ya Ilala wakati ule ilijenga Barabara ya Mombasa- Mazini-Moshi Bar na kipindi hiki barabara hii imeharibika sana hasa kipande cha kuanzia pale Mombasa mpaka Transfoma. Je, Serikali haioni ni wakati sasa kufanya ukarabati wa dharura wa kipande kile cha barabara ili kuwapunguzia wananchi kero?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba ni kweli barabara ile ilijengwa na sasa hivi kwa kweli imeharibika kutokana na adha za mvua. Nimhakikishie Mbunge tu kwamba, tunawaagiza watu wa TARURA, Mkoa wa Dar es Salaam waende wakafanye tathmini na kutafuta fedha kwa ajili ukarabati wa barabara hiyo. Ahsante. (Makofi)