Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA K.n.y. MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia msaada wa kisaikolojia watu waliopitia ukatili wa kijinsia?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwanza nishukuru majibu yake ni mazuri sana, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza, nina matarajio kwamba sasa kila Mkoa utapata kituo hiki cha One Stop Center. Swali langu, ni lini vituo hivi vitaanza?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Maafisa Ustawi wa Jamii ndio wanaotoa huduma za kisaikolojia; nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba mnaajiri Maafisa Ustawi wa Jamii wa kutosha ili waweze kutoa huduma hii?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Tendega kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuratibu uanzishaji wa vituo vya mkono kwa mkono hadi kufikia lengo la kuwa na angalau kituo kimoja kwa kila Mkoa. Hii ni kwa sababu ya kuwasaidia wananchi wetu pale wanapopata matatizo au changamoto ili waweze kwenda mahali ambapo watafanikiwa na kutatuliwa matatizo yao.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, Serikali itaendelea kuwaajiri Maafisa Ustawi wa Jamii kila tunapopata kibali ili waweze kusambazwa nchi nzima na kuhakikisha matatizo yote yanaondoka kwa wananchi na kupata elimu ambayo itawasaidia ili wasiathirike na msongo wa mawazo, ahsante. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA K.n.y. MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia msaada wa kisaikolojia watu waliopitia ukatili wa kijinsia?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa kuwa hivi vitendo vya ukatili wa kijinsia vimekuwa vikiongezeka nchini, na tumetambua huo mkakati wa Serikali kuhakikisha vituo na kuajiri ustawi wa jamii, lakini nataka nijue sasa mkakati kabisa wa kuhakikisha kwamba tunaondoa kabisa huu ukatili wa kijinsia. Mkakati gani ambao Serikali inao kuhakikisha kwamba, yani kunakuwa na zero ukatili wa kijinsia Tanzania?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, natambua kuwa kuna vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya wanawake na watoto hapa nchini. Jukumu letu ni kuhakikisha wanawake na watoto wanaofanyiwa vitendo hivyo vya ukatili kuwapatia huduma muhimu ikiwemo ushauri nasaha ili wasiathirike kiakili pale wanapopata vitendo vya ukatili, ahsante. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri sana ambayo ameyatoa Mheshimiwa Naibu Waziri kuhakikisha jamii nzima inashirikiana katika jambo hili la kutokomeza ukatili wa watoto, wanawake na makundi maalum nchini, lakini nadhani Bunge lako tukufu linafahamu kwamba Serikali inao mpango mkakati wa kitaifa wa kutokomeza unyanyasaji wa makundi haya maalum ambao ni jumuishi kwa sekta zote, na kila Wizara imeshirikishwa katika kuhakikisha mkakati huo maarufu kwa MTAKUWA unafanikiwa na unazaa matunda ya kuhakikisha Taifa hili la Tanzania linakuwa mstari wa mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata hivyo tumeshuhudia Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan yeye mwenyewe kwa kuzingatia matakwa ya kimataifa amekuwa mstari wa mbele kutengeneza afua ambazo zitasaidia mapambano hayo dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia katika Taifa letu. (Makofi)