Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, lini soko la samaki Mbamba Bay litaanza kutumika?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wazee wa Wilaya ya Nyasa walipokutana tarehe 5 Machi, 2023, waliniagiza na walisema kwamba wanaona Wilaya ya Nyasa inadharaulika kwa sababu miradi yake inachelewa kupatikana na ikianza haiishi kwa wakati na hata kama ikionesha dalili ya kuisha haipewi vifaa vinavyotakiwa.

Je, Serikali haioni haya mawazo ya wazee wa Wilaya ya Nyasa yana ukweli kiasi fulani? (Makofi)

Swali la pili, kwa kuwa pia kulikuwa kumejengwa karakana kwa ajili ya kutengeneza boti toka mwaka 2015 mpaka leo karakana hiyo haifanyi kazi iliyokusudiwa. Je, ni lini sasa na hiyo karakana itaweza kufanya kazi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Jambo la kwanza nitambue maoni ya Mheshimiwa Mbunge ambayo yametolewa na wazee wake na nimhakikishie tu kwamba Serikali haidharau wananchi wa Nyasa wala wananchi katika maeneo yoyote yale. Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ndiyo maana tumemuelezea kwanza katika jibu la msingi, kuhakikisha kwamba soko hilo linafunguliwa na ndiyo maana zabuni imeshafunguliwa. Tunamaliza tu mchakato atakwenda atajenga na baada ya kujenga tutalifungua soko hilo ili liweze kuhudumia wananchi wa Jimbo la Nyasa kupitia Ziwa Nyasa.

Mheshimiwa Spika, suala la karakana na lenyewe basi tumelipokea, mimi mwenyewe binafsi nitafanya hiyo jitihada binafsi ya kuhakikisha inafunguliwa kwa wakati. Ahsante sana.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, lini soko la samaki Mbamba Bay litaanza kutumika?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ningependa kufahamu ni lini Serikali mtapeleka fedha kumalizia ujenzi wa soko la Samaki Kata ya Mkinga, toka mmeahidi mwaka jana hakuna kitu kinaendelea?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Tunatambua kuhusu mahitaji ya Soko la Mkinga na tuliahidi katika bajeti. Changamoto ambayo ilikuwepo ni kwamba fedha zilikuwa hazijatoka lakini jambo hilo liko katika mpango na nafikiri Wizara ya Fedha itakapokuwa imeleta fedha kwa wakati huu, tutazileta kwa wakati na kuhakikisha soko hilo linajengwa.