Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Mohamed Chuachua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. RASHID M. CHUACHUA aliuliza:- Sera ya Serikali ya kujenga zahanati kwa kila kijiji na kituo cha afya kwa kila kata haijatekelezwa vyema katika Jimbo la Masasi ambapo hakuna kata yenye kituo cha afya cha Serikali na zahanati zilizopo ni saba tu:- (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa zahanati na vituo vya afya katika kata 14 za Jimbo la Masasi? (b) Je, Serikali inaweza kukiri kuwa kuna haja ya kuzipandisha hadhi Zahanati za Chisegu, Mumbaka na Mwenge Mtapika ili ziwe na vituo vya afya na hatimaye kuipunguzia mzigo Hospitali ya Mkomaindo pamoja na kusogeza huduma kwa jamii?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID M. CHUACHUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo. Swali la kwanza, mwaka 2014 baadhi ya watumishi wa hospitali ya Mkomaindo walifanya ubadhirifu wa shilingi milioni 29 za dawa. Je, Serikali imechukua hatua gani mpaka sasa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Jimbo la Masasi linakabiliwa na uhaba mkubwa sana wa watumishi wa huduma ya afya takribani watumishi 400. Je, Serikali haioni kwamba suala hili linapaswa kuchukuliwa kuwa ni la dharura ili watumishi hawa wapelekwe haraka iwezekanavyo katika Jimbo la Masasi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri wazi miongoni mwa maeneo ambayo nilitembelea ilikuwa ni Masasi nikiwa na Mbunge huyu na pale nilibaini changamoto kubwa na nilitoa maagizo mbalimbali. Hata hivyo, hivi sasa Ofisi yetu ya Rais, TAMISEMI, inafanya mchakato mpana siyo kuhusu suala la madaktari peke yake au idara ya afya peke yake kwa sababu kuna tatizo kubwa katika maeneo mengi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeunda timu hapa si muda mrefu itakuwa kule site vizuri ili kubaini upungufu wote siyo Masasi Mjini hali kadhalika na Masasi Vijijji. Tuna ripoti inayoonesha kwamba hali ya afya ya pale siyo sawasawa hasa kutokana na baadhi ya Wakuu wa Idara kushindwa kutimiza wajibu wao. Kwa hiyo, naomba nimweleze Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili tumekuwa serious nalo na tunaenda kulifanyia kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, siku tutakayokuja kuwachukulia hatua baadhi ya watendaji wazembe, tunaomba sana Waheshimiwa Wabunge waache kuleta vi-memo kwamba yule ni ndugu yangu, tutakwenda kuwashughulikia wale wanaoharibu fedha za Serikali na kwa hili tuko serious sana na wala hatuna masihara. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala la watumishi, Waziri wa Afya alishasema hapa mchakato unaendelea. Nimelisema jibu hili mara kadhaa, eneo hili la Masasi nimefika na nimeona mwenyewe Hospitali yetu ya Mkomaindo pale changamoto ni kubwa ikiwa ni pamoja na zahanati zetu, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo katika watu ambao wanaajiriwa hivi sasa, Masasi itapewa kipaumbele kupunguza tatizo hili kubwa la watumishi katika eneo hilo.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. RASHID M. CHUACHUA aliuliza:- Sera ya Serikali ya kujenga zahanati kwa kila kijiji na kituo cha afya kwa kila kata haijatekelezwa vyema katika Jimbo la Masasi ambapo hakuna kata yenye kituo cha afya cha Serikali na zahanati zilizopo ni saba tu:- (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa zahanati na vituo vya afya katika kata 14 za Jimbo la Masasi? (b) Je, Serikali inaweza kukiri kuwa kuna haja ya kuzipandisha hadhi Zahanati za Chisegu, Mumbaka na Mwenge Mtapika ili ziwe na vituo vya afya na hatimaye kuipunguzia mzigo Hospitali ya Mkomaindo pamoja na kusogeza huduma kwa jamii?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Mpanda Vijijini ni jimbo ambalo lina kata 16, kati ya hizo tatu tu ndizo ambazo zina vituo vya afya. Napenda kumuuliza swali Naibu Waziri, ni lini itajenga vituo vya afya katika Kata ya Mnyagala, Kasekese, Mpanda Ndogo, Tongwe, Bulamata, Ilangu, Ipwaga na Katuma?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Jimbo la Mheshimiwa Kakoso lina tatizo kubwa sana na ukiangalia ni jimbo ambalo zamani lilikuwa likigawanyika na bahati mbaya resources zao zimekuwa ni changamoto kubwa. Siyo tatizo la zahanati tu lakini hata suala zima la ambulance wana tatizo, hilo nalifahamu vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mchakato wetu hivi sasa na Wabunge ni mashahidi, wafanye reference kutoka katika Halmashauri zao, tumetuma barua kutoka TAMISEMI kuwaelekeza wabainishe changamoto za miundombinu hasa katika zahanati na vituo vya afya na kuwapa maelekezo jinsi Serikali inavyojipanga katika mkakati mpana wa kutatua tatizo la afya hasa katika suala zima la ujenzi wa zahanati.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu kubwa ni kwamba Mkurugenzi wa Jimbo la Mheshimiwa Kakoso na Madiwani watakuwa wanafanya harakati hizo kubainisha ili Serikali iweze kujipanga kwa kuwa na mpango mpana wa kutatua tatizo la ukosefu wa vituo vya afya katika nchi yetu. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Kakoso kwamba sasa hivi yuko Bungeni lakini waraka uko kule na watu wako site hivi sasa kubainisha changamoto hizo kwa ajili ya mpango mpana wa Serikali ili kutatua tatizo hilo.

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RASHID M. CHUACHUA aliuliza:- Sera ya Serikali ya kujenga zahanati kwa kila kijiji na kituo cha afya kwa kila kata haijatekelezwa vyema katika Jimbo la Masasi ambapo hakuna kata yenye kituo cha afya cha Serikali na zahanati zilizopo ni saba tu:- (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa zahanati na vituo vya afya katika kata 14 za Jimbo la Masasi? (b) Je, Serikali inaweza kukiri kuwa kuna haja ya kuzipandisha hadhi Zahanati za Chisegu, Mumbaka na Mwenge Mtapika ili ziwe na vituo vya afya na hatimaye kuipunguzia mzigo Hospitali ya Mkomaindo pamoja na kusogeza huduma kwa jamii?

Supplementary Question 3

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa tatizo la Masasi linafanana na Jimbo la Nsimbo na sasa hivi taasisi nyingi za Serikali zina masalia ya fedha, mojawapo ikiwa ni Tume ya Taifa ya Uchaguzi imerudisha shilingi bilioni 12. Je, Serikali ina mpango gani wa hizi fedha zinazobakia katika bajeti hii ya 2015/2016 katika moja ya Majimbo kutuletea kujenga vituo vya afya na zahanati kama Jimbo la Nsimbo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mpango wa Serikali kuhusu pesa zinazobakia, kwanza naomba nimjulishe kwamba hizi pesa kubakia ni kutokana na uongozi mzuri wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Kwa mara ya kwanza tunaona fedha zinarudishwa Serikalini kutatua matatizo ya wananchi. Naomba nilipongeze na Bunge lako hili kuhakikisha zile pesa zinarudi Serikalini na sisi Wabunge wote tutapata madawati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, siwezi kusema kwamba pesa zilizorudi zitaenda Nsimbo, isipokuwa kwa mtazamo mpana wa Mheshimiwa Rais ataangalia jinsi gani ya kutatua changamoto za wananchi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hasa katika ajenda kubwa ya kubana matumizi na kuwapelekea wananchi huduma ya msingi. Kwa hiyo, nadhani tunaangalia kwa ukubwa wake, lakini Rais ataelekeza vizuri nini cha kufanya katika nchi yetu, kipaumbele ni nini ili wananchi wapate huduma bora.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. RASHID M. CHUACHUA aliuliza:- Sera ya Serikali ya kujenga zahanati kwa kila kijiji na kituo cha afya kwa kila kata haijatekelezwa vyema katika Jimbo la Masasi ambapo hakuna kata yenye kituo cha afya cha Serikali na zahanati zilizopo ni saba tu:- (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa zahanati na vituo vya afya katika kata 14 za Jimbo la Masasi? (b) Je, Serikali inaweza kukiri kuwa kuna haja ya kuzipandisha hadhi Zahanati za Chisegu, Mumbaka na Mwenge Mtapika ili ziwe na vituo vya afya na hatimaye kuipunguzia mzigo Hospitali ya Mkomaindo pamoja na kusogeza huduma kwa jamii?

Supplementary Question 4

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Naomba nimuulize swali dogo tu Mheshimiwa Waziri. Kwa kuwa swali la msingi linafanana sana na Jimbo langu la Manyoni Magharibi ambapo kuna zahanati tatu tu. Je, ni lini Serikali itaanza kujenga vituo vya afya katika Kata za Idodyandole, Aghondi, Sanjaranda, Majengo, Tambuka Reli, Kitaraka, Mgandu, Kalangali, Mwamagembe na Ipande?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu Jimbo la Mheshimiwa Mbunge ni sehemu ambazo zimegawanyika na wana changamoto ya resources lakini suala la ujenzi wa hizi zahanati kama nilivyosema ajenda yetu ileile. Bahati mbaya mwaka huu tulikuwa na mchakato mpana wa vikao vyetu vya Bunge na vikao vya bajeti vya Halmashauri havijaenda vizuri, lakini niwaombe tunapoanza Bunge hili la Awamu ya Tano sisi Wabunge tuwe ndiyo wa kwanza kubainisha vipaumbele vya maeneo yetu na ujenzi huu wa zahanati maana yake unaanzia kwetu sisi, Mbunge unaangalia priority yako iko katika maeneo gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu kubwa ni kwamba, michakato ile itakapoanza katika vikao vyetu ikifika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, jukumu letu ni kusukuma sasa mambo haya yaweze kwenda vizuri. Najua wazi kwamba Mheshimiwa Mbunge wangu wa Manyoni ni kweli ana changamoto kubwa, lakini namuahidi kwamba mwaka huu ni wa kwanza tulikuwa na changamoto kubwa sana lakini mwaka unaokuja tutakaa pamoja; kama Wabunge tutakuwa katika mikutano yetu katika Halmashauri na sisi Ofisi ya TAMISEMI tutashirikiana vizuri zaidi kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya afya hususani kupata zahanati na vituo vya afya katika maeneo hayo aliyoyaeleza.